Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 11 Sitting 59 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 496 2018-06-27

Name

Allan Joseph Kiula

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Mashariki

Primary Question

MHE. JUSTIN J. MONKO (K.n.y MHE. ALLAN J. KIULA) aliuliza:-
Wilaya ya Mkalama ina vituo vya afya vitatu ambavyo vinakabiliwa na changamoto za uhaba wa watumishi, vipimo, majengo huku idadi ya wakazi wanaohitaji huduma ikiongezeka:-
a) Je, ni lini Serikali itaongeza idadi ya watumishi wa kada zote za kitaaluma katika vituo hivyo?
b) Je, ni lini Serikali itazipandisha hadhi zahanati kubwa ziwe Vituo vya Afya ili kuhudumia wananchi wengi zaidi kutoka Iguguno, Ilanda Msiu na Mkiko?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE) alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba nijibu swali la Mheshimiwa Allan Kiula, Mbunge wa Mkalama, lenye sehemu
(a) na (b) kama ifuatavyo:-
(a) Mheshimiwa Naibu Spika, katika mwaka wa fedha 2017/2018, Serikali imeajiri watumishi wa afya 2,534 kwenye hospitali za Wilaya, vituo vya afya na zahanati nchini. Kati ya hao, Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama ilipata watumishi 12. Vilevile Serikali inakamilisha ajira za watumishi wa afya 6,018 ambao wataajiriwa katika hospitali za wilaya, vituo vya afya na zahanati. Maeneo yenye upungufu vikiwemo Vituo vya Afya vya Mkalama vitawekwa katika kipaumbele cha kupatiwa watumishi.
(b) Mheshimiwa Naibu Spika, kipaumbele cha Serikali kwa sasa ni kuboresha vituo vya afya vilivyopo ili viweze kutoa huduma bora kwa wagonjwa badala ya kupandisha hadhi zahanati zilizopo. Katika Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama, Serikali imejenga Kituo cha Afya Kinyambuli kilichogharimu shilingi milioni 400 ili kuboresha huduma za dharura na upausuaji kwa mama wajawazito.