Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Justin Joseph Monko

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Singida Kaskazini

Primary Question

MHE. JUSTIN J. MONKO (K.n.y MHE. ALLAN J. KIULA) aliuliza:- Wilaya ya Mkalama ina vituo vya afya vitatu ambavyo vinakabiliwa na changamoto za uhaba wa watumishi, vipimo, majengo huku idadi ya wakazi wanaohitaji huduma ikiongezeka:- a) Je, ni lini Serikali itaongeza idadi ya watumishi wa kada zote za kitaaluma katika vituo hivyo? b) Je, ni lini Serikali itazipandisha hadhi zahanati kubwa ziwe Vituo vya Afya ili kuhudumia wananchi wengi zaidi kutoka Iguguno, Ilanda Msiu na Mkiko?

Supplementary Question 1

MHE. JUSTIN J. MONKO: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, naomba kuuliza maswali mawili madogo ya nyongeza. Swali la kwanza, ni kweli Serikali imeweza kufanikiwa kujenga kituo kama alivyosema kilichogharimu shilingi milioni 400 katika Wilaya ya Mkalama, lakini Wilaya ile inahitaji vituo vingi vya afya na yapo majengo ambayo wananchi tayari wameshaanza kuyajenga na yamefikia katika kiwango cha kupaua. Je, Serikali iko tayari sasa kuja kukamilisha kituo kingine cha afya ili wananchi waweze kupata huduma bora? (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, katika Jimbo la Singida Kaskazini tunavyo vituo viwili vya afya. Kituo cha Mgori na Kituo cha Ilongero na vituo hivi havijapata fedha za ukarabati na havifanyi upasuaji ukizingatia kwamba Halmashauri yangu haina hospitali. Je, Serikali iko tayari sasa kutoa fedha kwa ajili ya kuboresha vile vituo vianze kutoa huduma ya upasuaji na wananchi wa Jimbo la Singida Kaskazini waweze kupata huduma? (Makofi). Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante.

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE): Mheshimiwa Naibu Spika, ni ukweli ambao uko dhahiri na sisi Waheshimiwa Wabunge wote ni mashuhuda jinsi ambavyo Serikali imetilia maanani suala zima la afya kwa maana ya kujenga vituo vya afya pamoja na hospitali za Wilaya pamoja na kuziboresha Hospitali za Rufaa.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba, kwa kadri bajeti itakavyokuwa inaruhusu hii kasi ambayo tumeianza siyo ya nguvu za soda, tutaendelea nayo kuhakikisha kwamba tunaboresha masuala mazima ya afya ikiwemo katika Jimbo la Mkalama.
Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Monko ni shuhuda kwamba hivi karibuni Kituo chake cha Afya cha Mgori kimepelekewa pesa. Hii yote ni kuonesha jinsi ambavyo Serikali inajali afya za wananchi na jinsi ambavyo inaboresha huduma za afya. Naomba awe na subira kwa kushirikiana na Serikali hakika tutapiga hatua mbele zaidi.

Name

Athumani Almas Maige

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tabora Kaskazini

Primary Question

MHE. JUSTIN J. MONKO (K.n.y MHE. ALLAN J. KIULA) aliuliza:- Wilaya ya Mkalama ina vituo vya afya vitatu ambavyo vinakabiliwa na changamoto za uhaba wa watumishi, vipimo, majengo huku idadi ya wakazi wanaohitaji huduma ikiongezeka:- a) Je, ni lini Serikali itaongeza idadi ya watumishi wa kada zote za kitaaluma katika vituo hivyo? b) Je, ni lini Serikali itazipandisha hadhi zahanati kubwa ziwe Vituo vya Afya ili kuhudumia wananchi wengi zaidi kutoka Iguguno, Ilanda Msiu na Mkiko?

Supplementary Question 2

MHE. ALMAS A. MAIGE: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana nami kuniruhusu niulize swali la nyongeza kwenye swali hili 496. Kwa vile Jimbo zima la Tabora Kaskazini lina kituo kimoja tu cha afya na Mheshimiwa Rais alipopita katika Jimbo langu aliambiwa tatizo hili na akachangia shilingi milioni 10 ili kujenga Kituo cha Afya pale Mwagelezi na Mbunge akachangia shilingi milioni tano. Je, Serikali iko tayari kutuongeza hela ili kituo kile kikamilike? Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. (Makofi)

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE): Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza naomba kwa dhati kabisa nipongeze juhudi ambazo Mheshimiwa Mbunge amekuwa akizifanya kwa kushirikiana na wananchi wake. Jana tumepokea barua yake ambayo inaonesha jinsi ambavyo amechangia kutoka Mfuko wa Jimbo na pia katika kutoka vyanzo vyake katika suala zima la kuhakikisha afya inaboreshwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nimhakikishie, kwa jitihada na nguvu ambazo ameanzisha pamoja na wananchi wake, kwa kadri nafasi itakavyoruhusu na bajeti ikiruhusu hakika hatutasahau kuhakikisha kwamba tunapeleka huduma ya afya. Kama ambavyo amekuwa akisema kwamba siku hizi mzigo mzito humbebeshi Mnyamwezi unampunguzia unataka kila mtu abebe wa kwake, naomba nimhakikishie kwamba ni azma ya Serikali kuhakikisha kwamba huduma ya afya Uyui inaboreshwa. (Makofi)

Name

Cecil David Mwambe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ndanda

Primary Question

MHE. JUSTIN J. MONKO (K.n.y MHE. ALLAN J. KIULA) aliuliza:- Wilaya ya Mkalama ina vituo vya afya vitatu ambavyo vinakabiliwa na changamoto za uhaba wa watumishi, vipimo, majengo huku idadi ya wakazi wanaohitaji huduma ikiongezeka:- a) Je, ni lini Serikali itaongeza idadi ya watumishi wa kada zote za kitaaluma katika vituo hivyo? b) Je, ni lini Serikali itazipandisha hadhi zahanati kubwa ziwe Vituo vya Afya ili kuhudumia wananchi wengi zaidi kutoka Iguguno, Ilanda Msiu na Mkiko?

Supplementary Question 3

MHE. CECIL D. MWAMBE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi kwa ajili ya kuuliza swali kwenye Wizara hii. Mheshimiwa Naibu Waziri atakumbuka wakati wa ziara ya Waziri Mkuu Jimbo la Ndanda kwa maana ya Mkoa wa Mtwara alitembelea Kituo cha Afya cha Chiwale ambacho alikizindua siku ile.
Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na yote, Kituo cha Afya cha Chiwale kina uhaba mkubwa sana wa watumishi na barua tulishaipeleka toka mwezi wa Tatu kwa Waziri wa Utumishi, Mheshimiwa Mkuchika, nafikiri kwa kushirikiana na idara yake na Mheshimiwa Waziri Mkuu alisema, pamoja na kufungua kituo kile cha afya mara moja atahakikisha watumishi wameletwa pale kwa ajili ya kupunguza tatizo lililoko pale. Je, ni lini sasa Wizara itapeleka hao watumishi Kituo cha Afya cha Chiwale?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE): Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kwamba kuna suala zima la upungufu wa watumishi kwa upande wa afya na hivi karibuni Ofisi ya Rais, TAMISEMI imetangaza nafasi kwa ajili ya kuajiri watumishi wa afya ili kujaribu kupunguza pengo hilo.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge mchakato uko kwenye hatua za mwisho kabisa, haitapita mwezi kazi hii itakuwa imeshakamilika. Namwomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge katika maeneo ambayo kuna upungufu mkubwa tutazingatia kuhakikisha kwamba watumishi wanapalekwa ikiwa ni pamoja na kituo chake cha afya.

Name

Aysharose Ndogholi Mattembe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JUSTIN J. MONKO (K.n.y MHE. ALLAN J. KIULA) aliuliza:- Wilaya ya Mkalama ina vituo vya afya vitatu ambavyo vinakabiliwa na changamoto za uhaba wa watumishi, vipimo, majengo huku idadi ya wakazi wanaohitaji huduma ikiongezeka:- a) Je, ni lini Serikali itaongeza idadi ya watumishi wa kada zote za kitaaluma katika vituo hivyo? b) Je, ni lini Serikali itazipandisha hadhi zahanati kubwa ziwe Vituo vya Afya ili kuhudumia wananchi wengi zaidi kutoka Iguguno, Ilanda Msiu na Mkiko?

Supplementary Question 4

MHE. AISHAROSE N. MATEMBE: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza. Kwa kuwa Hospitali ya Wilaya ya Iramba ina changamoto kubwa hususani kwa watumishi na vifaatiba. Je, Serikali ina mpango gani wa kupeleka haraka watumishi na wataalam katika afya ya uzazi wa mpango? Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. (Makofi)

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE): Mheshimiwa Naibu Spika, kwa ujumla wake Mkoa wa Singida wamekuwa wakipigania suala zima la afya na jana nimejibu swali la Mheshimiwa Mbunge huyu ambaye leo ameuliza swali la nyongeza. Naomba nimhakikishie, kama nilivyotoa majibu alivyouliza Mheshimiwa Mwambe, mchakato wa ajira uko kwenye hatua za mwisho na lengo ni kuhakikisha kwamba maeneo yale yote ambayo yana upungufu yanapelekewa watumishi. Naomba Mheshimiwa Mbunge avute subira, zoezi likikamilika tutapeleka watumishi wa upande wa afya ili kupunguza hizo changamoto.

Name

Eng. James Fransis Mbatia

Sex

Male

Party

NCCR-Mageuzi

Constituent

Vunjo

Primary Question

MHE. JUSTIN J. MONKO (K.n.y MHE. ALLAN J. KIULA) aliuliza:- Wilaya ya Mkalama ina vituo vya afya vitatu ambavyo vinakabiliwa na changamoto za uhaba wa watumishi, vipimo, majengo huku idadi ya wakazi wanaohitaji huduma ikiongezeka:- a) Je, ni lini Serikali itaongeza idadi ya watumishi wa kada zote za kitaaluma katika vituo hivyo? b) Je, ni lini Serikali itazipandisha hadhi zahanati kubwa ziwe Vituo vya Afya ili kuhudumia wananchi wengi zaidi kutoka Iguguno, Ilanda Msiu na Mkiko?

Supplementary Question 5

MHE. JAMES F. MBATIA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Miaka mitatu mfululizo iliyopita Madaktari wamekuwa wakihitimu vyuo vyetu vikuu vya humu ndani. Madaktati wako wanasubiri ajira na sekta ya afya ina upungufu wa zaidi ya asilimia 50 ya Madaktari katika vituo mbalimbali na sekta nzima. Je, kwa nini Serikali isi-fast truck ili Madaktari hawa walioko mitaani wakaingia kwenye utumishi?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE): Mheshimiwa Naibu Spika, ni ukweli kwamba tuna uhitaji mkubwa wa Madaktari, lakini pia atakubaliana na mimi kwamba Ofisi ya Rais, TAMISEMI imetangaza nafasi na kama hilo halitoshi na Wizara ya Afya nayo imetangaza nafasi kwa ajili ya hao Madaktari na Wauguzi kwa ujumla wake. Naomba nimhakikishie kwamba mchakato upo pazuri, kwa hiyo, hicho ambacho anaulizia kuhusiana na suala zima la ku-fast truck ingekuwa tumechelewa wakati ule lakini kwa sasa hivi tuko hatua za mwisho, naomba avute subira hili litakamilika.