Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 11 Sitting 9 Natural Resources and Tourism Wizara ya Maliasili na Utalii 75 2018-04-13

Name

Augustino Manyanda Masele

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbogwe

Primary Question

MHE. AUGUSTINO M. MASELE aliuliza:-
Pori la Akiba la Kigosi Moyowosi linakabiliwa na tatizo sugu la kutokuwa na barabara za uhakika kwa ajili ya shughuli za utalii na doria.
• Je, ni lini Serikali italifufua greda aina ya katapila lenye namba za usajili ST 892 lililosimama kufanya kazi tangu mwaka 2015 ili lisaidie kukarabati barabara?
• Kwa kuwa gari aina ya Grand Tiger linalotumika kwa shughuli za utawala limekufa, je, ni lini gari hilo litatengenezwa au kuleta gari lingine ili lisaidie shughuli za utawala katika Pori la Kigosi Moyowosi?

Name

Japhet Ngailonga Hasunga (CPA)

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vwawa

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Maliasili na Utalii, ninaomba kujibu swali la Mheshimiwa Augustino Manyanda Masele, Mbunge wa Mbogwe, lenye sehemu (a) na (b) kwa pamoja, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, Wizara yangu inatambua umuhimu wa barabara na miundombinu mingine katika hifadhi zetu ili kuimarisha utalii na kufanya kazi za doria ipasavyo. Kwa kutambua umuhimu huo, Serikali iliamua kufufua mtambo, hususani greda lililokuwa limeharibika kwa muda mrefu katika Pori la Akiba la Moyowosi Kigosi ili liendelee kutumika kuimarisha barabara zilizopo ndani ya pori hilo. Greda hilo aina ya katapila lenye namba za usajili ST 892 limetengenezwa na linafanya kazi.
Aidha, Wizara ipo katika harakati za kufufua gari aina ya Grand Tiger ambalo hutumika kwa shughuli za utawala katika Pori la Akiba Moyowosi Kigosi ambapo mafundi wameshafanya tathmini ya ubovu wa gari hilo na Serikali imeshatenga fedha kwa ajili ya matengenezo hayo.