Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Augustino Manyanda Masele

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbogwe

Primary Question

MHE. AUGUSTINO M. MASELE aliuliza:- Pori la Akiba la Kigosi Moyowosi linakabiliwa na tatizo sugu la kutokuwa na barabara za uhakika kwa ajili ya shughuli za utalii na doria. • Je, ni lini Serikali italifufua greda aina ya katapila lenye namba za usajili ST 892 lililosimama kufanya kazi tangu mwaka 2015 ili lisaidie kukarabati barabara? • Kwa kuwa gari aina ya Grand Tiger linalotumika kwa shughuli za utawala limekufa, je, ni lini gari hilo litatengenezwa au kuleta gari lingine ili lisaidie shughuli za utawala katika Pori la Kigosi Moyowosi?

Supplementary Question 1

MHE. AUGUSTINO M. MASELE: Mheshimiwa Mwenyekiti, namshukuru sana Naibu Waziri kwa majibu yake mazuri sana. Kwanza niishukuru Serikali kwa kutengeneza hilo greda ambalo sasa kwa kweli litasaidia sana katika utengenezaji wa barabara kule kwenye Mapori yetu ya Akiba ya Kigosi Moyowosi. Sasa niombe kuuliza maswali mawili madogo ya nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la kwanza, je, Serikali ina mpango gani wa kuipatia mapori haya ya akiba pesa kwa ajili ya miradi ya maendeleo ya barabara katika mwaka ujao wa fedha ujao?
Mheshimiwa Mwenyekiti, la pili, kwa kuwa gari la Grand Tiger sasa hivi limeharibika na mapori haya mawili ni makubwa sana, je, Serikali iko tayari sasa kuyapatia haya mapori magari mawili kwa ajili ya kufanya doria na utawala katika maeneo hayo?

Name

Japhet Ngailonga Hasunga (CPA)

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vwawa

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nimpongeze kwa kazi kubwa ambayo umekuwa ukiifanya. Nakumbuka mwaka jana swali hilihili aliuliza na amekuwa akilifuatilia kwa karibu sana, hongera sana.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nimhakikishie tu Mheshimiwa Mbunge kwamba kwa sababu tumeshalitengeneza lile greda sasa hivi tumeshatenga fedha za kutosha kwa ajili ya kukarabati na kutengeneza miundombinu mbalimbali katika ile hifadhi. Kwa hiyo, pale bajeti itakapowasilishwa ataona ni kiasi gani tutakuwa tumetenga katika hilo eneo kwa ajili ya kufanya hiyo kazi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili kuhusu maombi ya gari; ni kweli kabisa hili gari ambalo nimesema kwamba tunaendelea kulitengeneza bado lina changamoto na tutalifufua. Lakini kwa nyongeza zaidi naomba nikuahidi kwamba tutakuongezea gari lingine moja ili yakiwa hayo mawili basi yataweza kufanya kazi nzuri sana katika hilo eneo. (Makofi)

Name

Juma Selemani Nkamia

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chemba

Primary Question

MHE. AUGUSTINO M. MASELE aliuliza:- Pori la Akiba la Kigosi Moyowosi linakabiliwa na tatizo sugu la kutokuwa na barabara za uhakika kwa ajili ya shughuli za utalii na doria. • Je, ni lini Serikali italifufua greda aina ya katapila lenye namba za usajili ST 892 lililosimama kufanya kazi tangu mwaka 2015 ili lisaidie kukarabati barabara? • Kwa kuwa gari aina ya Grand Tiger linalotumika kwa shughuli za utawala limekufa, je, ni lini gari hilo litatengenezwa au kuleta gari lingine ili lisaidie shughuli za utawala katika Pori la Kigosi Moyowosi?

Supplementary Question 2

MHE. JUMA S. NKAMIA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa nafasi na mimi niweze kuuliza swali moja la nyongeza.
Kwa kuwa Pori la Hifadhi ya Swagaswaga ambalo lipo karibu na Dodoma lina wanyama wengi na kwa kuwa Dodoma sasa ni Makao Makuu ya nchi. Je, Wizara haioni sasa ipo haja ya kuliimarisha pori hili ili liwe sehemu ya kivutio kikubwa cha utalii kwa wageni wanaokuja katika Mkoa wa Dodoma?

Name

Japhet Ngailonga Hasunga (CPA)

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vwawa

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Maliasili na Utalii naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Juma Nkamia...(Kicheko) Kama ifuatavyo; samahani nimekosea jina lako.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kwamba pori hili la Swagaswaga ni pori muhimu sana katika Mkoa huu wa Dodoma na hasa kwa kuzingatia kwamba sasa hizi hapa imekuwa ni Makao Makuu ya nchi. Kwa hiyo, tutachukua hatua mbalimbali za kuimarisha ili iwe ni kivutio cha utalii katika hili eneo na kuliwekea mikakati ya kutosha kusudi wananchi wengi ambao wanaishi katika Jiji hili la Dodoma waweze kutembelea katika hili eneo. Nikuhakikishie, kesho nitaenda kutembelea lile Pori la Mkungunero. Nikipata muda Jumapili nitapitia kwenye hilo eneo lingine ili tuone ni mikakati gani inaweza kufanyika tuweze kuimarisha utalii katika hili eneo.

Name

Daniel Nicodemus Nsanzugwako

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kasulu Mjini

Primary Question

MHE. AUGUSTINO M. MASELE aliuliza:- Pori la Akiba la Kigosi Moyowosi linakabiliwa na tatizo sugu la kutokuwa na barabara za uhakika kwa ajili ya shughuli za utalii na doria. • Je, ni lini Serikali italifufua greda aina ya katapila lenye namba za usajili ST 892 lililosimama kufanya kazi tangu mwaka 2015 ili lisaidie kukarabati barabara? • Kwa kuwa gari aina ya Grand Tiger linalotumika kwa shughuli za utawala limekufa, je, ni lini gari hilo litatengenezwa au kuleta gari lingine ili lisaidie shughuli za utawala katika Pori la Kigosi Moyowosi?

Supplementary Question 3

MHE. DANIEL N. NSANZUGWANKO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Mimi narudi kwenye swali la msingi. Ikolojia ya Kigosi Moyowosi inategemea sana uwepo wa Mto Malagarasi. Mto huu uko kwenye kitisho kikubwa cha kukauka kwa sababu mifugo imekuwa ni mingi. (Makofi)
Je, Wizara mnafanya nini kuokoa chepechepe (wetland) ya Mto Malagarasi ambayo imevamiwa na ng’ombe wengi na mpaka leo kuna ng’ombe zaidi ya 100,000 kwenye wetland ya Mto Malagarasi?

Name

Japhet Ngailonga Hasunga (CPA)

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vwawa

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana kwa swali la Mheshimiwa Daniel Nsanzugwanko. Naomba nimhakikishie tu kwamba katika lile eneo la Mto Malagarasi ni eneo muhimu sana kwa ajili kutoa maji na kusambaza katika maeneo muhimu kama ulivyokuwa umesema wewe mwenyewe. Ni kweli kabisa sasa hivi tunaweka jitihada, limevamiwa lile pori, kuna wanyama wengi, kuna mifugo mingi emeenda katika lile eneo, lakini lile eneo ni mojawapo ya maeneo ambayo yako kwenye Ramsar sites.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, hivi sasa tunakuja na mkakati wa kutosha kabisa wa kuweza kuhakikisha kwamba hatua ya kwanza ilikuwa ni kuweka vigingi katika mipaka yetu ile Ramsar site. Bado zoezi halijakamilika, litakapokamilika naamini kabisa tutakuwa tumekuja na ufumbuzi kidogo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hatua ya pili, nitumie fursa hii kabisa kwamba mifugo hairuhusiwi katika maeneo ya hifadhi zozote kwa mujibu wa sheria. Ndiyo maana tukikamata hiyo mifugo, kwa kweli tunaipeleka mahakamani na hatua kali zitachukuliwa kwa watu wa namna hiyo.
Kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba tutachukua hatua za makusudi za kuhakikisha kwamba mifugo yote katika eneo hilo inaondolewa mara ili kuhakikisha huo mto unaendelea kuwepo na uendelee kutusaidia katika matumizi mbalimbali.

Name

Marwa Ryoba Chacha

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Serengeti

Primary Question

MHE. AUGUSTINO M. MASELE aliuliza:- Pori la Akiba la Kigosi Moyowosi linakabiliwa na tatizo sugu la kutokuwa na barabara za uhakika kwa ajili ya shughuli za utalii na doria. • Je, ni lini Serikali italifufua greda aina ya katapila lenye namba za usajili ST 892 lililosimama kufanya kazi tangu mwaka 2015 ili lisaidie kukarabati barabara? • Kwa kuwa gari aina ya Grand Tiger linalotumika kwa shughuli za utawala limekufa, je, ni lini gari hilo litatengenezwa au kuleta gari lingine ili lisaidie shughuli za utawala katika Pori la Kigosi Moyowosi?

Supplementary Question 4

MHE. MARWA R. CHACHA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante.
Katika hifadhi Serengeti National Park pamoja na Ngorongoro, hali ya barabara siyo mzuri na hususan kwenye kipande cha barabara kuanzia Ngorongoro getini mpaka lango la Serengeti National Park kuna udongo wa Volcano ambao hata watengeneze vipi, kwa muda mfupi unakuta ule udongo unaharibika.
Mheshimiwa Mwenyekiti, je, Serikali haina mpango wowote wa kutengeneza ile barabara hata kwa kiwango cha zege ili kuondoa shida kubwa ambayo tunaipata watu tunaopita kwenye hiyo barabara?

Name

Japhet Ngailonga Hasunga (CPA)

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vwawa

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nampa hongera sana, amekuwa ni mdau mkubwa sana kwa sababu maeneo mengi, maliasili na hifadhi nyingi ziko katika eneo lake. Nafikiri nitakapokwenda kule, nitajua maeneo hayo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nimhakikishie tu Mheshimiwa Mbunge kwamba sasa hivi Serikali inapitia maombi mbalimbali, inapitia utaratibu wa kuweka barabara ya kudumu ambayo inaanzia Karatu kupitia Ngorongoro mpaka Serengeti. Mara baada ya taratibu hizo kukamilika na clearance zote kufanyika, kwa sababu ni maeneo ya hifadhi, kumekuwa na mabishano makubwa juu ya aina ya barabara ambayo inatakiwa ijengwe.
Sasa hivi tumefikia hatua nzuri, makubaliano yanakuja na ninaamini kabisa kwamba baada ya muda mfupi tutaanza kuweka barabara ya kudumu ambayo ndiyo suluhu ya hilo tatizo ambao Mheshimiwa Mbunge amelisema.

Name

Rwegasira Mukasa Oscar

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Biharamulo Magharibi

Primary Question

MHE. AUGUSTINO M. MASELE aliuliza:- Pori la Akiba la Kigosi Moyowosi linakabiliwa na tatizo sugu la kutokuwa na barabara za uhakika kwa ajili ya shughuli za utalii na doria. • Je, ni lini Serikali italifufua greda aina ya katapila lenye namba za usajili ST 892 lililosimama kufanya kazi tangu mwaka 2015 ili lisaidie kukarabati barabara? • Kwa kuwa gari aina ya Grand Tiger linalotumika kwa shughuli za utawala limekufa, je, ni lini gari hilo litatengenezwa au kuleta gari lingine ili lisaidie shughuli za utawala katika Pori la Kigosi Moyowosi?

Supplementary Question 5

MHE. OSCAR R. MUKASA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Tumeshuhudia namna ambavyo Naibu Waziri anasisitiza kwa ukali kabisa kuchukuliwa hatua watu wanaoingiza mifugo hifadhini jambo ambalo ni sawa. Lakini anaongea kwa sauti ya chini na unyonge inapofikia kufidia mwananchi anayeharibiwa mazao na wanyama. Sasa kwa sababu Biharamulo asilimia 50 karibu ya eneo ni hifadhi na kwa sababu vijiji zaidi ya 15 kila mara wanaharibiwa mazao yao, yuko tayari twende tutathimini? Inawezekana akiona hali ile atajua namna Serikali ikae kutafuta namna ya kubadilisha approach ili tuwafidie wananchi badala ya kuwapa kifuta jasho? (Makofi)

Name

Japhet Ngailonga Hasunga (CPA)

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vwawa

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kabisa katika maeneo yale ya Biharamulo sehemu kubwa ni hifadhi na kumekuwa na changamoto mbalimbali hasa zikiwemo hizo za mifugo pamoja na uharibifu na uvamizi katika maeneo haya ya vijiji. Naomba nimhakikishie tu kwamba niko tayari wakati wowote tupange twende tukaangalie tuone ni maeneo gani na tuone mikakati gani tunaweza tukaifanya kwa kushirikiana na Serikali tuone hatua za kuchukua. Ahsante sana. (Makofi)