Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 11 Sitting 37 Natural Resources and Tourism Wizara ya Maliasili na Utalii 314 2018-05-25

Name

Ester Amos Bulaya

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ESTER A. BULAYA aliuliza:-
Vijiji vya Tamau, Nyantwali, Serengeti, Mcharo, Kanzugu, Bukore na Mihale Wilaya ya Bunda vinapakana na Hifadhi ya Serengeti lakini havinufaiki na chochote kutoka katika hifadhi husika.
Je, ni utaratibu gani umeandaliwa na Mamlaka ya Hifadhi ya Wanyamapori ili kusaidia vijana wanaozunguka hifadhi kupatiwa ajira ili kunufaika na hifadhi husika kama njia mojawapo ya kudumisha ujirani mwema?

Name

Japhet Ngailonga Hasunga (CPA)

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vwawa

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Maliasili na Utalii, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Ester Amos Bulaya, Mbunge wa Bunda Mjini, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, Hifadhi ya Taifa ya Serengeti inapakana na Wilaya nane ambazo ni Ngorongoro, Meatu, Itilima, Bariadi, Busega, Tarime, Bunda na Serengeti. Aidha, Wilaya ya Bunda ina vijiji sita vinavyopakana moja kwa moja na hifadhi ambavyo ni Serengeti, Nyatwali, Tamau, Balili, Kuzungu na Bukore. Aidha, vijiji vya Mihale na Bukore vinapakana na pori la Akiba la Ikorongo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika mwaka wa fedha 2017/2018 hifadhi imetenga jumla ya shilingi 32,233,180 kuchangia ujenzi wa madarasa mawili katika shule ya msingi Bunyunyi, Kijiji cha Hunywari.
Mheshimiwa Mwenyekiti, aidha, Halmashauri ya Wilaya ya Bunda inaendelea kukusanya tozo za huduma yaani hotel levy kwenye hoteli na lodges katika hifadhi zilizopo kwenye eneo la utawala la Wilaya hiyo. Mchango wa hifadhi katika Wilaya ya Bunda kutoka mwaka 2004/2005 hadi mwaka 2017/2018 ni shilingi 276,720,630 ambazo zimetumika kutekeleza jumla ya miradi tisa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na miradi ya ujirani mwema, Wizara imekuwa ikichangia katika Halmashauri ya Wilaya ya Bunda asilimia 25 ya mapato yanayotokana na ada ya shughuli za uwindaji wa kitalii zinazofanyika katika mapori ya Akiba ya Ikorongo na Gurumeti.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika kipindi cha mwaka 2004/2005 hadi 2014/2015 Halmashauri wa Wilaya ya Bunda ilipokea jumla ya shilingi 156,200,125.87. Katika kipindi cha mwaka 2016/2017 na 2017/2018 yaani kuanzia juni mwaka 2017 hadi Januari 2018 Halmashauri ya Wilaya ya Bunda imepokea jumla ya shilingi 77,559,441.84.