Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Ester Amos Bulaya

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ESTER A. BULAYA aliuliza:- Vijiji vya Tamau, Nyantwali, Serengeti, Mcharo, Kanzugu, Bukore na Mihale Wilaya ya Bunda vinapakana na Hifadhi ya Serengeti lakini havinufaiki na chochote kutoka katika hifadhi husika. Je, ni utaratibu gani umeandaliwa na Mamlaka ya Hifadhi ya Wanyamapori ili kusaidia vijana wanaozunguka hifadhi kupatiwa ajira ili kunufaika na hifadhi husika kama njia mojawapo ya kudumisha ujirani mwema?

Supplementary Question 1

MHE. ESTER A. BULAYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niulize maswali mawili madogo ya nyongeza.
Kwanza Mheshimiwa Naibu Waziri mambo mengi wamekuongopea humu, siyo Wilaya wala Halmashauri ya Mji ambayo imewahi kunufaika na chochote kutokana na Mbuga ya Serengeti. The way walivyokujibu kama Bunda, kuna Halmashauri moja. Hivi vijiji vyote viko kwenye Halmashauri ya Mji na asubuhi nimetoka kuongea na Mkurugenzi na Mhasibu hatujawahi kupata hata shilingi moja. Ni lini sasa tutapata hii asilimia 25 ya tozo za uwindaji? Swali la kwanza. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, wananchi wanaozunguka Mbuga ya Serengeti katika Jimbo langu wamekuwa wakipata tatizo kubwa sana la tembo kuharibu mali zao na Mheshimiwa Jenista ameshajionea uharibifu huu. Takribani wananchi 880…
...kati ya hao waliolipwa ni 330 tu, bado watu 550 hawajalipwa kifuta jacho japo kidogo. Ni lini sasa watalipwa? (Makofi)

Name

Japhet Ngailonga Hasunga (CPA)

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vwawa

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza niseme kwamba ni kweli kabisa Wilaya ya Bunda ina Halmashauri mbili na haya majibu sisi tunayoyatoa tunatoa katika Wilaya, siyo katika Halmashauri. Tunatoa katika Wilaya nzima, tunazungumzia Wilaya. Kama ingekuwa kwamba labda inatakiwa tuangalie kwenye Halmashauri, basi majibu hayo yengefanana. Hayo majibu niliyoyasema na hizo fedha ambazo nimezisema ni zile zilizoletwa katika Wilaya nzima ya Bunda.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba sasa nijibu maswali yake kama ifuatavyo; kwa asilimia 25 na kwa kuwa Halmashauri yake ya Mji ina vijiji vinavyopakana na haya Mapori ya Akiba na hizi fedha nilizosema zimeshapelekwa, kama bahati mbaya Halmashauri yake haijapata mgao, basi tukitoka hapa nitafuatilia kuhakikisha ule mgawanyo unakwenda katika vijiji vyote vinavyohusika. Kwa hiyo, hilo nitalifanya. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, la pili, naomba nirekebishe kidogo takwimu, kwa takwimu sisi tulizonazo Mheshimiwa Mbunge, katika Wilaya ya Bunda, kifuta jasho kilicholipwa ni kwa wahanga 1,127 ambao jumla ya shilingi 186,333,350 zimelipwa kama kifuta jasho. Shilingi milioni moja zililipwa kama pole kwa mhanga mmoja ambaye alipoteza maisha.
Kwa hiyo, suala la kusema kwamba hazijatolewa, zimetolewa na katika list niliyonayo mpaka sasa hivi nimeangalia kama Bunda kuna wahanga ambao wanadai, bado sinayo. Kwa hiyo, kama wapo ambao bado wanadai, naomba hiyo list tuipate ili tuweze kuifanyia kazi kusudi waweze kulipwa mara moja. (Makofi)

Name

Leah Jeremiah Komanya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Meatu

Primary Question

MHE. ESTER A. BULAYA aliuliza:- Vijiji vya Tamau, Nyantwali, Serengeti, Mcharo, Kanzugu, Bukore na Mihale Wilaya ya Bunda vinapakana na Hifadhi ya Serengeti lakini havinufaiki na chochote kutoka katika hifadhi husika. Je, ni utaratibu gani umeandaliwa na Mamlaka ya Hifadhi ya Wanyamapori ili kusaidia vijana wanaozunguka hifadhi kupatiwa ajira ili kunufaika na hifadhi husika kama njia mojawapo ya kudumisha ujirani mwema?

Supplementary Question 2

MHE. LEAH J. KOMANYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipatia nafasi niulize swali la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Halmashauri ya Wilaya ya Meatu inapaswa kunufaika na miradi ya maendeleo inayotokana na ujirani mwema, Outreach Department kutokana na Serengeti National Park na Ngorongoro Conservation; lakini ni zaidi ya miaka kumi haujawahi kutekelezwa mradi wowote.
Je, ni lini sasa Halmashauri ya Meatu italetewa miradi ya maendeleo? (Makofi)

Name

Japhet Ngailonga Hasunga (CPA)

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vwawa

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kabisa kwamba taasisi zetu zote zinazohusika na masuala ya uhifadhi zinao mpango madhubuti kabisa wa kuhakikisha kwamba zinachangia katika miradi mbalimbali ya vijiji vile vinavyozunguka katika maeneo hayo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa Wilaya ya Meatu nina uhakika kabisa kwamba imetengewa kiasi cha fedha ambazo zitatekeleza miradi mbalimbali ya vile vijiji vinavyozunguka katika maeneo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, labda niwahakikishie Waheshimiwa Wabunge, tumekuwa tukifanya hivyo, kwa mfano, takribani kuanzia mwaka 2004 mpaka 2016 jumla ya shilingi bilioni 17.2 zimetumika katika kutekeleza miradi mbalimbali ya vijiji vinavyozunguka hifadhi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, nina uhakika na Wilaya ya Meatu ni mojawapo ambayo imefaidika na itaendelea kufaidika. Na mimi naomba tuwasiliane baadae ili tuone kwamba imetengewa kiasi gani katika mwaka unaofuata.

Name

Eng. James Fransis Mbatia

Sex

Male

Party

NCCR-Mageuzi

Constituent

Vunjo

Primary Question

MHE. ESTER A. BULAYA aliuliza:- Vijiji vya Tamau, Nyantwali, Serengeti, Mcharo, Kanzugu, Bukore na Mihale Wilaya ya Bunda vinapakana na Hifadhi ya Serengeti lakini havinufaiki na chochote kutoka katika hifadhi husika. Je, ni utaratibu gani umeandaliwa na Mamlaka ya Hifadhi ya Wanyamapori ili kusaidia vijana wanaozunguka hifadhi kupatiwa ajira ili kunufaika na hifadhi husika kama njia mojawapo ya kudumisha ujirani mwema?

Supplementary Question 3

MHE. JAMES F. MBATIA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana. Mkoa wa Kilimanjaro umezungukwa na vijiji 88 ambavyo ni vya ujirani mwema, lakini kwa miaka kumi iliyopita mapato ya mlima huu ilikuwa ni shilingi bilioni 471.5 lakini vijiji vinavyozunguka vimepata shilingi bilioni 2.28 tu ambayo ni chini ya asilimia 0.48 wakati sera ni asilimia 7.5.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali haioni umuhimu ili vijiji hivi vipate haki yake badala ya kupata shilingi bilioni 2.6 kwa mwaka, wapate shilingi bilioni 40, TANAPA waweze kukaa na Halmashauri husika za Rombo, Moshi na Hai ili waweke utaratibu ili waweze kupata haki yao inavyostahili? (Makofi)

Name

Japhet Ngailonga Hasunga (CPA)

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vwawa

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kabisa vijiji vingi vinapakana kabisa na ile hifadhi yetu ya Mlima Kilimanjaro na niseme tu kwamba katika utaratibu wa sera ya ujirani mwema, tunachokifanya sisi katika bajeti nzima ile ya TANAPA tunatenga kati ya asilimia tano mpaka asilimia saba kwa ajili ya kutekeleza miradi mbalimbali ile ya ujirani mwema.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hatukusema kwamba basi hizi zote asilimia saba ndiyo ziende katika vile vijiji, katika lile eneo husika. Maadam Mheshimiwa Mbatia ameleta haya mapedekezo, tutakaa chini, tutayaangalia na nitaiagiza TANAPA wakae na hizo Halmashauri ili kuona namna gani wanaweza kufaidi zaidi katika huo mradi. (Makofi)