Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 11 Sitting 41 Defence and National Service Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga taifa 347 2018-05-31

Name

Esther Nicholus Matiko

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MASOUD ABDALLAH SALIM (K.n.y. MHE. ESTHER M. MATIKO) aliuliza:-
Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) limejitwalia maeneo ya wananchi wa Kenyambi na Bugosi kinyume kabisa na sheria baada ya kukaribishwa kwa hifadhi ya muda kufuatia kukatika kwa mawasiliano kati ya kambi yao iliyopo Kata ya Nyandoto na Tarime Mjini:-
a) Je, ni kwa nini Serikali imeshindwa kuwalipa fidia wananchi hao waliochukuliwa ardhi yao na JWTZ tangu mwaka 2007?
b) Je, ni kwa nini JWTZ wasirudi kwenye kambi yao iliyopo Kata ya Nyandoto yenye eneo kubwa kuliko kuchukua maeneo yaliyo katikati ya makazi?

Name

Dr. Hussein Ali Mwinyi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kwahani

Answer

WAZIRI WA ULINZI NA JESHI LA KUJENGA TAIFA alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Esther Nicholas Matiko, Mbunge wa Tarime Mjini, lenye sehemu (a) na (b) kwa pamoja, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali kupitia Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa inatambua umuhimu wa kulipa fidia ya ardhi iliyotwaliwa. Uthamini kwa ajili ya fidia kwa wananchi umefanyika tangu mwaka 2013. Ufinyu wa bajeti ya Serikali ndiyo umechelewesha kufanyika kwa malipo ya fidia hiyo. Katika mwaka wa fedha 2017/2018, Serikali kupitia Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa ilitenga shilingi bilioni 20.03 kwa ajili ya ulipaji wa fidia na masuala mengine yanayoendana na upimaji wa maeneo. Naamini fedha hizo zikipatikana, ulipaji wa fidia ya ardhi utafanyika.
Mheshimiwa Mwenyekiti, eneo la Nyandoto lipo chini ya Halmashauri ya Wilaya ya Tarime. Mwaka 1992 Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania lilikabidhi eneo hilo kwa Halmashauri ya Wilaya ambayo imelipangia matumizi mengine.