Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 14 Sitting 1 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 2 2019-01-29

Name

Omar Abdallah Kigoda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Handeni Mjini

Primary Question

MHE. OMARI A. KIGODA aliuliza:-

Je, ni lini Serikali kupitia Halmashauri itakamilisha majengo ya madarasa yaliyotokana na nguvu za wananchi?

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. MWITA M. WAITARA) alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais - TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Omar Abdala Kigoda, Mbunge wa Handeni kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Serikali inatambua juhudi za wananchi na wadau wa maendeleo katika Sekta ya Elimu ikiwa ni pamoja na kusaidia ujenzi wa miundombinu ya shule kama vile vyumba vya madarasa, madawati, matundu ya vyoo, nyumba za Walimu, mabwalo na maabara.

Mheshimiwa Spika, Halmashauri ya Mji wa Handeni ina maboma yapatayo 15 ya vyumba vya madarasa yaliyoanza kwa nguvu za wananchi na kati ya hayo, maboma sita yako katika hatua ya lenta. Hadi Januari, 2019 Halmashauri imepokea jumla ya shilingi 46,600,000/= kwa ajili ya kukamilisha ujenzi wa maboma yaliyoanza kwa nguvu za wananchi ili yaanze kutumika.

Mheshimiwa Spika, Serikali kwa kushirikiana na Wadau kupitia Programu ya Lipa kwa matokeo (EP4R) na Programu ya kuimarisha ubora wa Elimu Tanzania (EQUIP-T) itaendelea kuweka kipaumbele na kutenga bajeti kwa ajili ya ukamilishaji wa maboma yaliyoanza kujengwa kwa nguvu za wananchi.

Aidha, Halmashauri zinahimizwa kuweka kipaumbele na kutenga bajeti kupitia mapato ya ndani kwa ajili ya ukamilishaji wa maboma yaliyopo kabla ya kuanzisha miradi mipya. Naomba kuwasilisha.