Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Omar Abdallah Kigoda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Handeni Mjini

Primary Question

MHE. OMARI A. KIGODA aliuliza:- Je, ni lini Serikali kupitia Halmashauri itakamilisha majengo ya madarasa yaliyotokana na nguvu za wananchi?

Supplementary Question 1

MHE. OMARI A. KIGODA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Kutokana na suala la elimu bure, imeleta changamoto ya kuwa wanafunzi wengi sana ambao wamejiandikisha, lakini kuna uhaba mkubwa sana wa Walimu ambao unasababisha hawa wanafunzi wasipate elimu bora: Je, Serikali ina mpango gani mkakati wa kuajiri Walimu wengi zaidi ili hawa wanafunzi waweze kupata elimu bora?

Mheshimiwa Spika, ahsante sana.

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. MWITA M. WAITARA):

Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Ni kweli kwamba elimu ya msingi bila malipo imeleta chachu ya maendeleo na mwamko mpya na wanafunzi wengi wamejiandikisha na kuingia katika mfumo wa elimu Tanzania. Hili ni jambo jema na kupongezwa kwa maamuzi thabiti ya Mheshimiwa Rais kwa Awamu ya Tano.

Mheshimiwa Spika, mpango uliopo ni kwamba tunao Walimu zaidi ya 11,000 katika Shule za Sekondari, ambao hawa tunaona kwamba mzigo wao siyo mkubwa sana, tumeomba kibali washushwe waje kufundisha Shule za Msingi ili waweze kuziba gap la uchache wa Walimu.

Mheshimiwa Spika, jambo la pili, kumekuwa na wale Walimu ambao wanastaafu na wengine wanapata makosa ya kinidhamu kazini na wengine wanafariki dunia, lakini hapa katikati kumekuwa na mkwamo kidogo, Mheshimiwa Rais amesharuhusu kuajiri angalau kila mwaka kupunguza gap hili.

Mheshimiwa Spika, mpango wa tatu, tumepata kibali cha kuajiri Walimu zaidi za 6,000 ambao wakiajiriwa watapunguza upungufu wa Walimu katika Shule zetu za Msingi. Ahsante sana.