Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 14 Sitting 1 Energy and Minerals Wizara ya Nishati 6 2019-01-29

Name

Prof. Jumanne Abdallah Maghembe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mwanga

Primary Question

MHE. PROF. JUMANNE A. MAGHEMBE aliuliza:-

Awamu ya III ya REA ilizinduliwa Wilayani Mwanga mnamo Julai, 2017 lakini hadi sasa utekelezaji wake haujaanza;

Je ni lini utekelezaji wa mradi huo utaanza?

Name

Subira Khamis Mgalu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nishati, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Profesa Jumanne Abdallah Maghembe, Mbunge wa Mwanga, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, utekelezaji wa mradi wa kusambaza umeme vijijini katika Wilaya ya Mwanga kupitia REA awamu ya tatu ulianza mwezi Oktoba, 2017 ukifanywa na Mkandarasi Kampuni ya Urban and Rural Engineering Service Limited. Katika mzunguzuko wa kwanza vijiji 14 vya Wilaya ya Mwanga vitapatiwa umeme vikiwemo Vijiji vya Ndorwe, Kinghare, Kigoningoni, Kiriche, Mangulai, Kirya, Lungurumo, Mangara, Kiverenge, Kichwa, Chang’ombe, Vuchama Ngofi na Ngujini.

Mheshimiwa Spika, kazi ya kupeleka umeme katika Vijiji vya Wilaya ya Mwanga inajumuisha ujenzi wa njia ya umeme ya msongo wa kilovoti 33 yenye urefu wa kilomita 10.98, njia ya umeme ya msongo wa kilovoti 0.4 yenye urefu wa kilomita 24, ufungaji wa transfoma 12 za KVA 50 pamoja na kuwaunganisha wateja wa awali 347. Kwa sasa mkandarasi anaendelea na kazi za awali ikiwemo uchimbaji wa mashimo na kusimika nguzo katika Kata ya Kirya. Kazi ya kupeleka umeme katika vijiji hivyo itakamilika mwezi Juni, 2019. Gharama ya mradi ni Sh.1,350,000,000.