Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 14 Sitting 3 Natural Resources and Tourism Wizara ya Maliasili na Utalii 29 2019-01-31

Name

Rashid Abdallah Shangazi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mlalo

Primary Question

MHE. RASHID A. SHANGAZI aliuliza:-

Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi yake ya kujenga geti la kuingilia Hifadhi ya Mkomazi katika Kijiji cha Kivingo?

Name

Constantine John Kanyasu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Geita Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII aljibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Maliasili na Utalii, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Rashid Abdallah Shangazi, Mbunge wa Jimbo la Mlalo, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Hifadhi ya Taifa Mkomazi ipo Wilaya za Same, Mwanga, Lushoto, Korogwe na Mkinga. Kwa sasa wageni wote wanaotembelea hifadhi hii hutumia lango la Zange lililopo katika Wilaya ya Same.

Mheshimiwa Spika, katika mpango na bajeti wa mwaka fedha 2019/2020, Shirika la Hifadhi za Taifa (TANAPA) limetenga fedha kwa ajili ya ujenzi wa lango la wageni katika eneo la Kamakota, jirani na Kijiji cha Kivingo Wilayani Lushoto. Lango hilo limetengewa kuhudumia wageni wanaotumia barabara ya Tanga – Lushoto - Mlalo - Kihurio na Same.

Mheshimiwa Spika, sanjari na ujenzi wa lango la wageni eneo la Kamakota, Shirika la Hifadhi za Taifa limeweka kwenye mpango wake maeneo yanyotarajiwa kuwekewa malango ambayo ni Njiro (Wilaya ya Same), Ndea (Wilaya ya Mwanga) na Umba (Wilaya ya Mkinga).