Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Rashid Abdallah Shangazi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mlalo

Primary Question

MHE. RASHID A. SHANGAZI aliuliza:- Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi yake ya kujenga geti la kuingilia Hifadhi ya Mkomazi katika Kijiji cha Kivingo?

Supplementary Question 1

MHE. RASHID A. SHANGAZI: Mheshimiwa Spika, ahsante. Pamoja na majibu ya Serikali yenye kutia matumaini, nina maswali mawili madogo ya nyongeza, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, swali la kwanza, kwa kuwa eneo hili la Mkomazi lina barabara ambayo inaunganisha utalii wa ukanda wa juu na ukanda wa chini kwa maana ya barabara ya Hekicho – Kwekanda - Lugulua, je, Wizara hii iko tayari kukaa na wenzetu wa TAMISEMI kupitia TARURA ili waweze kuboresha miundombinu wageni waweze kufika kwa urahisi katika geti hili ambalo tunakusudia kulifungua?

Mheshimiwa Spika, kwa kuwa Wilaya Lushoto ina vivutio vingi vya utalii na vingi bado havijatambulika ikiwemo utalii wa maliasili lakini pia na utamaduni ikiwemo makazi yale ya Chifu Kimweri, Waziri uko tayari kuongozana nami kwenda Lushoto ili angalau waweze kuvibaini vivutio hivi viweze kugeuka kuwa fursa ya kiuchumi kwa wananchi wa Lushoto?

Name

Constantine John Kanyasu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Geita Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Rashid Abdallah Shangazi, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, baada ya kuwahakikishia ufunguzi wa lango hili, TANAPA watashirikiana na TAMISEMI kuona
namna kurekebisha barabara hii ambayo Mheshimiwa Mbunge anaomba kutoka Hekicho kwenda Kwekanda ili kuweza kufungua pia lango la utalii kwenye maeneo haya ya misitu.

Mheshimiwa Spika, swali lake la pili kuhusu kuvitambua vivutio vya utalii ambavyo bado havijatambuliwa, niko tayari kuongozana na Mheshimiwa Mbunge kwenda kuangalia vivutio hivi na kuviweka kwenye package ya pamoja kuhamisha watu wa TANAPA waweze kuvitangaza.

Name

Dr. Stephen Lemomo Kiruswa Mamasita

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Longido

Primary Question

MHE. RASHID A. SHANGAZI aliuliza:- Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi yake ya kujenga geti la kuingilia Hifadhi ya Mkomazi katika Kijiji cha Kivingo?

Supplementary Question 2

MHE. DKT. STEVEN L. KIRUSWA: Mheshimiwa Spika, nashukuru sana kwa kunipa nafasi ya niweze kuuliza swali la nyongeza kwa Waziri wa Maliasili na Utalii.

Mheshimiwa Spika, kwa kuwa wananchi wa Wilaya ya Longido wanaoishi katika vijiji 32 vilivyopo Ukanda wa Magharibi unaokwenda mpaka Ziwa Natron waliungana wakatenga eneo la Hifadhi la Wanyamapori ambalo wameliita Lake Natron Wildlife Management Area, wakapita mchakato mzima na hatua zote za usajili ikabaki kipengele kimoja tu ambacho kipo katika dhamana ya Waziri ya kuwapatia user right yaani haki ya matumizi ya rasilimali ya wanyama pori katika eneo hili. Jumuiya hii imetumia rasilimali nyingi kupitia mchakato ambao wote mnaujua siyo wa bei nafuu na umetumia fedha za wafadhili na za Serikali, ni lini sasa Jumuiya hii itapewa user right wawe kuanza kulisimamia na kutumia rasilimali ya eneo hilo?

Name

Constantine John Kanyasu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Geita Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali Dkt. Kiruswa, Mbunge wa Longido, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, kuna mchakato mrefu sana wa kusajili WMA na kama Mheshimiwa Mbunge ananihakikishia kwamba taratibu zote za awali zimekwishatimia, nitakwenda kufuatilia na kuona kama kipengele kilichobaki kinamhusu Waziri peke yake basi nitamshauri Mheshimiwa Waziri kutoa hiyo user right.