Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 14 Sitting 6 Energy and Minerals Wizara ya Nishati 55 2019-02-04

Name

Daimu Iddi Mpakate

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduru Kusini

Primary Question

MHE. DAIMU I. MPAKATE aliuliza:-

Serikali imeweka zuio la kusafirisha shaba ghafi kabla ya kuchakatwa, jambo ambalo limesababisha uchimbaji mdogo wa Mbesa wa Shaba usimame na wachimbaji wadogo kukosa kazi za kufanya:-

Je, ni lini Serikali itajenga mtambo wa kuchenjua shaba katika Kijiji cha Mbesa?

Name

Subira Khamis Mgalu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MADINI alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Madini, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Daimu Iddi Mpakate, Mbunge wa Tunduru Kusini, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, ni kweli kuwa tarehe 3 Machi, 2017, Serikali iliweka zuio la kusafirisha nje ya nchi madini ghafi na kuelekeza madini yote yanayoongezewa thamani yaongezewe thamani hapa nchini. Zuio hilo lilikuwa na nia njema ya kutaka shughuli zote za uongezaji thamani madini zifanyike hapa nchini ili kuongeza manufaa kwa wananchi na Taifa kwa ujumla kutokana na rasilimali ya madini.

Mheshimiwa Spika, kutokana na zuio hilo, kuna GN Na. 60 ya mwaka huu, yaani tarehe 25, Januari, 2019, Serikali imetoa mwongozo wa kuhakiki uongezaji thamani madini au miamba nchini kabla ya madini hayo kupata kibali cha kusafirishwa kwenda nje ya nchi.

Mheshimiwa Spika, madini ya shaba yanapatikana katika maeneo mbalimbali nchini. Hivyo, kwa kuzingatia hilo, Serikali imepokea maombi ya kampuni 11 zenye nia ya kujenga vinu vya kuyeyusha madini hayo (smelters) baada ya kutangaza uwepo wa fursa hiyo. Serikali ipo katika hatua za mwisho za kuteua kampuni zitakazojenga smelters hizo ili kuwaondolea adha ya soko la madini hayo wachimbaji wadogo na wakubwa.