Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Daimu Iddi Mpakate

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduru Kusini

Primary Question

MHE. DAIMU I. MPAKATE aliuliza:- Serikali imeweka zuio la kusafirisha shaba ghafi kabla ya kuchakatwa, jambo ambalo limesababisha uchimbaji mdogo wa Mbesa wa Shaba usimame na wachimbaji wadogo kukosa kazi za kufanya:- Je, ni lini Serikali itajenga mtambo wa kuchenjua shaba katika Kijiji cha Mbesa?

Supplementary Question 1

MHE. DAIMU I. MPAKATE: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa majibu mazuri ya Serikali, ila nina maswali mawili ya nyongeza. moja ya Kampuni zilizoomba kujenga mtambo wa kuchenjua shaba pale Mbesa ni Metalicca Commodities Corporation ya Marekani ikishirikiana na Minerals Access System Tanzania (MAST) lakini ni muda mrefu toka wameomba na majibu hayatolewi kutokana na kuchelewa kwa mwongozo. Je, Serikali mpaka sasa imefikia wapi kutengeneza mwongozo mzuri ukizingatia shaba ina tabia tofauti na madini mengine ili kuwezesha wawekezaji hao walioomba kupata kibali cha kuweza kujenga mitambo yao?

Mheshimiwa Spika, swali la pili; kumekuwa na leseni nyingi sana za utafiti zilizotolewa na Serikali kwa kampuni tofauti mbalimbali kwa muda mrefu na wamekuwa wanakaa kwa muda mrefu bila kuweza kuendeleza maeneo hayo:-

Je, Serikali ina mpango gani wa kuwanyang’anya au kufuta leseni zile za utafiti kwa yale makampuni ambayo yamekaa muda mrefu na badala yake maeneo yale kupewa wachimbaji wadogo ili waweze kujikimu na kujitafutia riziki kwa njia ya kuchimba madini katika maeneo hayo? Ahsante.

Name

Subira Khamis Mgalu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MADINI: Mheshimiwa Spika, ni kweli kabisa kwamba Serikali imetoa mwongozo na mwongozo wenyewe umetoka tarehe 25, Januari, unaoonesha aina zote za madini yanaweza yakachenjuliwa katika kiwango gani na baada ya kuchenjuliwa yanapewa sasa ruhusa (permit) kwa ajili ya kusafirisha kupeleka nje ya nchi. Kwa hiyo, kwa kila aina ya madini tumetoa mwongozo huo.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, Mheshimiwa Mbunge afuatilie tu na aone kwamba sasa wale wawekezaji wanaokuja ambapo sisi tumejipanga kutafuta mwekezaji ambaye kweli yuko serious na kampuni zimekuja zaidi 11 wameonesha nia ya kuwekeza kwenye smelter, tunataka tuwawekee kampuni ambazo tuna uhakika nazo kwamba zinaweza kuwekeza kwenye kuchenjua au kuyeyusha zile shaba kwa maana ya smelter.

Mheshimiwa Spika, swali la pili, kuhusu hizi leseni za utafiti za makampuni mbalimbali, ni kwamba mpaka sasa hivi, katika meza zetu tunapitia leseni zote ambazo zinaonesha ni leseni zilizotolewa mwaka gani. Tunataka kuangalia status zake zikoje? Tunapitia leseni ambazo zinafanyiwa kazi; lakini zile leseni ambazo ni za PL walipewa makampuni mbalimbali, wengi tumeona wameshikilia maeneo na hawafanyi kazi yoyote. Sasa hivi Wizara yetu tunapitia leseni zote. Kwa kampuni ambayo haifanyi chochote katika leseni ambazo tumewapatia, tunakwenda kuzifuta.

Mheshimiwa Spika, hata hivyo, kwa leseni ambazo tumewapa watu kwa ajili ya uchimbaji kwa maana ya Primary Mining License, Mining License, Special Mining License na zenyewe tunaangalia kwa mujibu wa sheria na taratibu. Kama umekuwa na leseni huwezi kuifanyia kazi, sisi Wizara ya Madini muda siyo mrefu tutawapa default notice na tunakwenda kuzifuta leseni zote.

Mheshimiwa Spika, ahsante sana.