Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 session 13 Sitting 1 Energy and Minerals Wizara ya Nishati 10 2018-11-06

Name

Augustine Vuma Holle

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kasulu Vijijini

Primary Question

MHE. AUGUSTINO V. HOLLE aliuliza:-
Kwa muda mrefu Mkoa wa Kigoma umesubiri kuunganishwa kwenye Grid ya Taifa ya Umeme:-
Je, ni lini Serikali itaunganisha Mkoa huo kwenye Grid ya Taifa ya Umeme?

Name

Subira Khamis Mgalu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI NISHATI alijibu:-
Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nishati napenda kujibu swali la Mheshimiwa Augustino Vuma Holle, Mbunge wa Jimbo la Kasulu Vijijini, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, Serikali kupitia TANESCO mwezi Desemba, 2017 ilikamilisha upembuzi yakinifu kwa ajili ya kujenga njia ya kusafirisha umeme ili kuunganisha Mkoa wa Kigoma na Grid ya Taifa kutokea Tabora. Mradi unahusisha ujenzi wa njia ya umeme ya msongo kilovoti 132 kutoka Tabora hadi Kidahwe Mkoani Kigoma kupitia Urambo na Nguruka umbali wa kilomita 370. Kazi za mradi zinahusisha ujenzi wa vituo vya kupozea umeme vya 132/33 KV katika Miji ya Urambo na Nguruka. Gharama ya kazi hizo inakadiriwa kufikia Dola za Marekani 81,000,000 na ujenzi wa mradi unatarajia kuanza mwezi Machi, 2019 na kukamilika mwezi Juni, 2020.
Mheshimiwa Spika, Serikali kwa upande mwingine inatekeleza ujenzi wa mradi wa kusafisha umeme…
Mheshimiwa Spika, Serikali kwa upande mwingine inatekeleza ujenzi wa mradi wa kusafisha umeme wa North West Grid KV 400 Mbeya – Tunduma – Sumbawanga – Mpanda – Kigoma – Nyakanazi wenye urefu wa kilometa 1372. Mradi huu utawezesha kuyaunganisha maeneo ya Magharibi na Kaskazini Magharibi mwa Tanzania katika Grid ya Taifa na kuondoa matumizi ya mitambo ya mafuta katika maeneo hayo. Kwa sasa mikataba ya makubaliano ya fedha imesainiwa kati ya Tanzania na Benki ya Dunia pamoja na Benki ya Maendeleo ya Afrika na mradi utagharimu Dola za Kimarekani 455,000,000.
Mheshimiwa Spika, Serikali pia imeanza utekelezaji wa mradi wa kuzalisha umeme wa MW 45 kwa kutumia maporomoko ya maji ya Mto Malagarasi. Ujenzi wa mradi huo utaenda sambamba ujenzi wa wa njia ya kusafirisha umeme wa mgongo wa KV 132 yenye urefu wa kilometa 53 kutoka Malagarasi hadi Kidahwe Kigoma unatarajiwa kujengwa katika kipindi cha mwaka wa fedha 2019/2020 na kukamilika 2020/2021.