Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Augustine Vuma Holle

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kasulu Vijijini

Primary Question

MHE. AUGUSTINO V. HOLLE aliuliza:- Kwa muda mrefu Mkoa wa Kigoma umesubiri kuunganishwa kwenye Grid ya Taifa ya Umeme:- Je, ni lini Serikali itaunganisha Mkoa huo kwenye Grid ya Taifa ya Umeme?

Supplementary Question 1

MHE. AUGUSTINO V. HOLLE: Mheshimiwa Spika, kwanza nishukuru kwa majibu mazuri ya Naibu Waziri, lakini nina swali moja la nyongeza. Kwa kuwa kama Mkoa bado hatujaunganishwa kwenye Grid ya Taifa na kumekuwa na tatizo kubwa sana la kukosa nishati hii muhimu na kupelekea mkoa wetu kuwa miongoni mwa mikoa maskini; sasa je, Wizara ya Nishati imejipangaje vipi kuhakikisha kwamba inakamilisha kwa haraka na kwa ufanisi mradi wa REA awamu ya tatu katika Mkoa wa Kigoma ambao kimsingi umezinduliwa muda umeenda sana katika Kijiji au Kata ya Lusese? Ahsante.

Name

Subira Khamis Mgalu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Naomba nimpongeze sana Mheshimiwa Mbunge kwa kazi nzuri ya kufuatilia changamoto ya nishati. Ni kweli Mkoa wa Kigoma pamoja na Mkoa wa Katavi kazi za upelekaji umeme kupitia mradi wa REA awamu ya tatu mzunguko wa kwanza zilichelewa kutokana na matatizo ambayo yalikuwa nje ya uwezo wa Wizara yetu ya Nishati pamoja na Wakala wetu Vijijini. Hata hivyo mradi huo umeshazindua rasmi na mkandarasi anaendelea na kazi ya survey na watakamilisha hivi karibuni.
Mheshimiwa Spika,aomba niwatoe hofu wakazi wa Mkoa wa Kigoma pamoja na Katavi kwamba kwa kweli kwa maelekezo ya Serikali na mkandarasi aliyeteuliwa ana uwezo na hivyo atafanya kazi kwa haraka iwezekenavyo nakushukuru. (Makofi)

Name

Hussein Mohamed Bashe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Mjini

Primary Question

MHE. AUGUSTINO V. HOLLE aliuliza:- Kwa muda mrefu Mkoa wa Kigoma umesubiri kuunganishwa kwenye Grid ya Taifa ya Umeme:- Je, ni lini Serikali itaunganisha Mkoa huo kwenye Grid ya Taifa ya Umeme?

Supplementary Question 2

MHE. HUSSEIN M. BASHE: Mheshimiwa Spika, nashukuru na naomba kuuliza swali dogo la nyongeza. Pamoja na shukurani za dhati kwa niaba ya wananchi wa Nzega kwa kutatua tatizo la umeme katika chanzo cha maji katika Mji wa Nzega, Wizara ya Nishati nilitaka tu nipate kauli ya Waziri ama Naibu Waziri. Mradi wa REA Phase III katika Jimbo la Nzega unasuasua; mkandarasi ameonekana site mara moja alipokuwepo Waziri na kuweka nguzo. Hata hivyo mpaka sasa nguzo zile zimesimama vile vile na maeneo ambayo aliahidi kuwasha umeme mpaka leo hayajawashwa. Ni lini mradi huu utapata speed ambayo wananchi wa Jimbo la Nzega wanaitarajia?(Makofi)

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, kwanza nimpongeze Mheshimiwa Bashe anavyotupa ushirikiano kati ka kupeleka umeme kwenye Jimbo lake.
Mheshimiwa Spika, nitangulie tu kusema, kwa sasa Wakandarasi katika Jimbo la Nzega wanafanya kazi katika vijiji 11 na katika Jimbo la Mheshimiwa Bashe wanakamilisha kazi katika maeneo ya Migua karibu kabisa na Ziba katika Jimbo la Igunga. Kwa hiyo nimwambie tu Mheshimiwa Bashe kwamba vile vifaa vyote ambavyo vilikuwa vinasubiriwa kuja ikiwepo nyaya na transfoma vimeshafika tangu juzi; na sasa hivi katika Jimbo la Mheshimiwa Bashe kuna transifoma 12 zimewekwa juzi. kwa hiyo nimpe uhakika Mheshimiwa Bashe na wananchi wa Nzega kwamba kazi ya kupeleka umeme kwenye vijiji 32 katika Jimbo lake litakamilika kabla ya mwezi Julai mwaka ujao. (Makofi)

Name

Daniel Nicodemus Nsanzugwako

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kasulu Mjini

Primary Question

MHE. AUGUSTINO V. HOLLE aliuliza:- Kwa muda mrefu Mkoa wa Kigoma umesubiri kuunganishwa kwenye Grid ya Taifa ya Umeme:- Je, ni lini Serikali itaunganisha Mkoa huo kwenye Grid ya Taifa ya Umeme?

Supplementary Question 3

MHE. DANIEL N. NSANZUGWANKO: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Nina swali fupi sana la nyongeza kuhusu huu mradi wa Northwest Grid kutoka Mbeya – Tunduma mpaka Nyakanazi. Bunge hili tulishauri kwamba kwa sababu njia ni ndefu, takribani kilometa 2500, tulishauri kwamba angalau mkandarasi awe zaidi ya mmoja ili mmoja aweze kuanzia Kigoma kwenda Nyakanazi wakati mwingine anatoka Tunduma kuja Mpanda mpaka Kigoma. Maadam fedha zimepatikana sasa, je, ushauri huo umezingatiwa? Vinginevyo kitakachotokea ni kwamba itakuwa ni kazi ya muda mrefu kwa sababu njia ni ndefu sana. Ahsante sana.

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, pia nimpongeze Mheshimiwa Nsanzugwanko kwa swali hili muhimu sana katika ukanda wa Kusini na hasa Magharibi mwa upande wa Kigoma, Katavi pamoja na Iringa.
Mheshimiwa Spika, kwanza katika mradi huu ni kweli kwamba tumepata fedha kutoka Benki ya Dunia jumla dola milioni 455 ambayo itatekeleza mradi wa kusafirisha umeme mkubwa wa kilovott 400 kutoka Iringa kupita Mbeya hadi Sumbawanga. Taratibu za kuanza mradi katika portion hii zimeshaanza, ujenzi rasmi utaanza mwezi Machi mwakani.
Mheshimiwa Spika, kama ambavyo wanashauri Waheshimiwa Wabunge, na yeye akiwemo, mradi huu ni mrefu sana, una umbali wa kilometa 2872 ambapo tumeugawa katika portion tatu. Kutoka Iringa, Sumbawanga hadi Tunduma ni portion moja ambayo tutaanza mwezi Machi na kuanzia Mei utaanza kuanzia Sumbawanga hadi Mpanda na kutoka Mpanda hadi Nyakanazi.
Mheshimiwa Spika, lakini mbali na mradi huo, tumeona wananchi wa Katavi na Kigoma watachelewa sana kupata umeme wa gridi tumeanza kujenga mradi mwingine wa kutoka Ipole, Sikonge kupeleka kilovott 132 Katavi ili kurahisisha wananchi wa maeneo ya katikati kupata umeme wa grid mapema iwezekanavyo.
Mheshimiwa Spika, lakini vile vile mradi mwingine wa nne unaopeleka umeme wa grid katika Mkoa wa Kigoma ni pamoja na ule wa kutoka Tabora kupita Urambo hadi Kaliua umbali wa kilometa 370 nao uaanza kujengwa mwezi Februari mwaka ujao. Kwa hiyo ni matumaini yetu wananchi wa Katavi na Kigoma wataanza kupata umeme wa grid kuanzia mwezi Oktoba mwakani.