Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 session 13 Sitting 1 Energy and Minerals Wizara ya Nishati 11 2018-11-06

Name

Musa Rashid Ntimizi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Igalula

Primary Question

MHE. MUSA E. NTIMIZI aliuliza:-
Katika mradi wa kupeleka umeme vijijini, Jimbo la Igalula limepitiwa na umeme katika baadhi ya maeneo ya Kata za Kigwa, Igalula, Goweko na Nsolola tu kati ya Kata kumi na moja za Jimbo hilo:-
a) Je, Serikali ina mpango gani wa kupeleka umeme katka Kata na Vijiji vya Jimbo la Igalula vilivyobaki?
b) Katika Kata ya Igalula, Kijiji cha Igalula ambapo kuna bwawa la maji kuna hitaji la nguzo kumi tu kwa ajili ya kusaidia kusukuma mitambo ya maji. Je, Serikali itasaidiaje kupeleka nguzo hizo ili kutatua tatizo hilo?

Name

Subira Khamis Mgalu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI alijibu:-
Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nishati, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Musa Rashid Ntimizi, Mbunge wa Jimbo la Igalula, lenye sehemu (a) na (b), kama ifuatavyo:-
(a) Mheshimiwa Spika, Serikali inaendelea na utekelezaji wa miradi ya kupeleka umeme vijijini kupitia mradi wa REA III mzunguko wa kwanza. Katika Jimbo la Igalula lililopo Wilayani yui jumla ya vijiji 98 vitanufaika na Mradi wa REA III. Kupitia mradi huu jumla ya vijiji 25 vitaunganishiwa umeme. Aidha, vijiji 73 vilivyobaki vitapatiwa umeme kupitia REA III Mzunguko wa Pili utakaoanza kutekelezwa Mwezi Julai, 2019 na kukamilika Mwezi Juni, 2021.
Mheshimiwa Spika, kwa sasa mkandarasi kampuni ya Intercity Builders Limited anaendelea na kazi za ujenzi wa miundombinu ya kusambaza umeme katika vijiji vya Kata za Ibelamilundi, Ibiri, Kigwa, Goweko, Nsololo na Igalula. Aidha, vijiji vya Kigwa B, Goweko Market, Goweko Tambukareli, Goweko Juu, Imalakaseko, Igalula I na Igalula II vilipatiwa umeme kupitia Mradi wa REA Awamu ya Pili uliokamilika mwezi Desemba, 2016.
Mheshimiwa Spika, kazi ya Mradi wa REA III unaondelea sasa katika Jimbo la Igalula zinajumuisha ujenzi wa njia ya msongo wa kilovott 33 yenye urefu wa kilometa 66.79; njia ya umeme wa msongo wa killovot 0.4 yenye urefu wa kilometa 102.242; ufungaji wa transforma 34; pamoja na kuwaunganishia umeme wateja wa awali 2,235. Gharama ya mradi huu ni shilingi bilioni 6.62.
(b) Mheshimiwa Spika, katika Kata ya Igalula ambako kuna bwawa la maji, TANESCO imeshakamilisha kazi na umeme umeshawashwa katika kituo cha pampu ya maji. Ahsante.