Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 14 Sitting 9 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 102 2019-02-07

Name

Innocent Sebba Bilakwate

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kyerwa

Primary Question

MHE. INNOCENT S. BILAKWATE aliuliza:-

Wilaya ya Kyerwa ina Vituo vitatu vya Afya, lakini kituo kimoja ndicho kina uhakika wa kutoa huduma, vilevile kuna uhaba wa watumishi ambao wanafanya kazi kwenye mazingira magumu pamoja na ukosefu wa nyumba za watumishi:-

Je, Serikali ipo tayari kutenga fedha kwa ajili ya ujenzi wa Hospitali ya Wilaya na nyumba za watumishi ili kutekeleza Ilani ya CCM na kuondoa adha wanayoipata akina mama, watoto na wananchi wengine kwa ujumla?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE) alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Innocent Seba Bilakwate, Mbunge wa Kyerwa, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Halmashauri ya Wilaya ya Kyerwa ina jumla ya Vituo vya Huduma za Afya 32 vinavyohudumua watu takribani 394,375. Kati ya vituo hivyo, kuna Vituo vya Afya vitatu, vyote vikiwa vya Serikali, Zahanati ziko 28; 23 za Serikali na tano ni za watu binafsi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, Halmashauri ya Wilaya ya Kyerwa ni miongoni mwa Halmashauri 67 nchini zilizopatiwa shilingi bilioni 1.5 kila moja kwa ajili ya ujenzi wa Hospitali ya Wilaya. Mpaka sasa hatua za awali za ujenzi zinaendelea na ujenzi wa awamu ya kwanza unatarajiwa kukamilika Juni 30, 2019. Vilevile Serikali imepeleka kiasi cha shilingi milioni 800 kwa ajili ya ujenzi na upanuzi wa Vituo vya Afya Murongo na Kamuli katika Halmashauri ya Wilaya ya Kyerwa ambapo mpaka sasa ujenzi umekamilika kwa asilimia 98.