Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 15 Sitting 2 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 9 2019-04-03

Name

Ahmed Ally Salum

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Solwa

Primary Question

MHE. EZEKIEL M. MAIGE (K.n.y. MHE. AHMED A. SALUM) aliuliza:-

Waziri Mkuu alipofanya ziara katika Mkoa wa Shinyanga aliahidi ujenzi wa Vituo viwili vya Afya katika Jimbo la Solwa:-

Je, ni lini ahadi hiyo itatekelezwa?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE) alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Ahmed Ally Salum, Mbunge wa Solwa kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Serikali inaendelea kutekeleza Ilani ya Chama cha Mapinduzi ya mwaka 2015 inayoelekeza kuwa na Kituo cha Afya kila Kata sambamba na utekelezaji wa ahadi mbalimbali za viongozi wa Kitaifa. Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga yenye Jimbo la Solwa ilipewa kipaumbele na kutengewa shilingi milioni 900.0 kwa ajili ujenzi na ukarabati wa Kituo cha afya Tinde, kilichogharimu shilingi milioni 400 na Kituo cha Afya Samuye kilichogharimu shilingi milioni 500. Vituo hivyo vimekamilika na vimeanza kutoa huduma kwa wananchi. Aidha, Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga ni miongoni mwa Halmashauri 67 zilizoidhinishiwa shilingi bilioni 1.5 kwa ajili ya ujenzi wa Hospitali ya Halmashauri. Fedha zote zimepokelewa na ujenzi unaendelea.

Mheshimiwa Spika, nimhakikishie Mheshimiwa Ahmed Ally Salum Mbunge wa Solwa kuwa ahadi za viongozi zitaendelea kutekelezwa kwa awamu kulingana na upatikanaji wa fedha.