Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 15 Sitting 2 Energy and Minerals Wizara ya Nishati 11 2019-04-03

Name

Lucy Simon Magereli

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. LUCY S. MAGERELI aliuliza:-

Wilaya ya Kigamboni inakabiliwa na tatizo la msongo mdogo wa umeme na matukio ya kukatika umeme ya mara kwa mara hata mara tatu kwa siku:-

Je, Serikali ina mpango gani wa kukomesha tatizo hilo?

Name

Subira Khamis Mgalu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nishati, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Lucy Simon Magereli, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, ni kweli kumekuwa na tatizo la umeme kupungua nguvu (low voltage) katika maeneo ya Manispaa ya Mji wa Kigamboni kutokana na uchakavu wa mifumo ya umeme pamoja na kuongezeka kwa mahitaji ya umeme kutokana na kasi ya ujenzi wa nyumba za makazi na viwanda. Serikali kupitia TANESCO inaendelea na kazi ya kuboresha hali ya umeme (voltage improvement) kwa kuongeza njia za umeme na transformer katika maeneo ya Kigamboni yakiwemo Vijibweni, Kibugumo, Kibada, Uvumba, Kisota, Maweni na Kwa Thoma.

Katika kushughulikia tatizo hili, Serikali kupitia TANESCO mwaka 2017 ilifanya matengenezo kwa ajili ya kuboresha Kituo cha Kupooza Umeme Kigamboni kwa kukiongezea uwezo wake kutoka MVA 5 iliyokuwa inahudumia wateja 3000 kufikia MVA 15 yenye uwezo wa kuhudumia wateja 12,000. gharama ya mradi ni shilingi 1,500,000,000/=.

Mheshimiwa Spika, Serikali ipo katika hatua za mwisho za kukamilisha ujenzi wa Kituo Kipya cha Kupooza Umeme cha Kurasini cha 132/33KV kitakachopeleka umeme wa uhakika katika maeneo ya Kigamboni. Ujenzi wa kituo hicho ulianza mwaka 2018 na utakamilika mapema mwezi Aprili, 2019 na hivyo kuboresha hali ya upatikanaji wa umeme Kigamboni.

Mheshimiwa Spika, katika hatua nyingine Serikali kupitia TANESCO inaendelea na kazi ya ujenzi wa njia ya kusafirisha umeme msongo wa kilovoti 132 kutoka Kurasini hadi Dege na ujenzi wa kituo kipya cha kupoza umeme cha MVA 120 katika eneo la Dege Kigamboni. Mradi huu ulianza kutekelezwa kuanzia mwezi Januari, 2018 kwa gharama ya shilingi bilioni 16 na utakamilika ifikapo Septemba, 2019. Kukamilika kwa mradi huu kutaimarisha na kuboresha hali ya upatikanaji wa umeme katika maeneo ya Mbagala na Kigamboni na hivyo kulipatia ufumbuzi wa kudumu tatizo la kukatika umeme kwa Wilaya za Kigamboni na Temeke. Ahsante.