Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Lucy Simon Magereli

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. LUCY S. MAGERELI aliuliza:- Wilaya ya Kigamboni inakabiliwa na tatizo la msongo mdogo wa umeme na matukio ya kukatika umeme ya mara kwa mara hata mara tatu kwa siku:- Je, Serikali ina mpango gani wa kukomesha tatizo hilo?

Supplementary Question 1

MHE. LUCY S. MAGERELI: Mheshimiwa Spika, nashukuru sana kwa kuwa Mheshimiwa Waziri amekiri mwenyewe kwamba tatizo hili lipo Kigamboni na ni kubwa. Katika majibu yake unaona anaeleza kabisa kwamba umeme unaopatikana Kigamboni unakidhi kuhudumia wateja 12,000 tu, wakati wakazi wa Kigamboni ni zaidi ya 300,000.

Mheshimiwa Spika, nimekuwa nikifuatilia suala hili tangu mwaka 2016 Mheshimiwa Muhongo akiwa Waziri wa Nishati, majibu ni haya haya. Mheshimiwa Mgalu yeye ni shahidi, nimeshakutana naye mara kadhaa tukijadiliana suala hili hili na majibu yamekuwa ni haya haya. Je Serikali ina nia thabiti ya kuondoa tatizo hili Kigamboni kweli?

Mheshimiwa Spika, swali la pili, katika majibu yake Mheshimiwa Waziri ameonesha kwamba kuna ujenzi wa kituo cha kupoza umeme cha Kurasini cha KVA 132, ambacho anaeleza kwamba kinakamilika mapema Aprili, 2019. Tunavyozungumza leo ni mapema Aprili, 2019, je, kituo hiki kimekwishakamilika?

Name

Subira Khamis Mgalu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI NISHATI: Mheshimiwa Spika, katika swali lake la kwanza la nyongeza, Mheshimiwa Mbunge amesema kwamba majibu ni yale yale na nini mkakati wa Serikali. Nataka nimthibitishie Mheshimiwa Mbunge majibu si yale yale kwa sababu zipo hatua zinazoendelea na tatizo la kukatikakatika kwa umeme hususan siyo Kigamboni tu katika Jiji la Dar es Salaam, ni kutokana na kuongezeka kwa mahitaji na kuzidiwa kwa kituo cha Ubungo cha jumla. Nini Serikali imefanya; yapo matengenezo makubwa pia yanaendelea pale Ubunge ambapo kwa sasa kituo kile ambacho kilikuwa na uwezo wa kusafirisha umeme wa megawati 635 kwa ujumla kwa Mkoa wa Dar es Salaam na mahitaji yake ni megawati 500 lakini inapotokea kwa mfano kituo cha Songas, kituo cha Tegeta, kinapotokea matengenezo ya mtambo mojawapo lazima kunakuwa na upungufu wa umeme katika maeneo mbalimbali ikiwepo Kigamboni.

Mheshimiwa Spika, hata hivyo, kwenye jibu langu la msingi nimesema kwamba hatua zilizochukuliwa zaidi ya bilioni 16 zimewekezwa katika kituo cha Dege; zaidi ya bilioni 1.5 zishatumika. Kwa hiyo, nataka nimthibitishie Mheshimiwa Mbunge nia ya dhati ipo na si kwa Kigamboni tu, bali kwa maeneo mbalimbali ya Mkoa wa Dar es Salaam na maeneo mengine.

Mheshimiwa Spika, swali lake la pili Mheshimiwa Mbunge dada Lucy anaulizia kwamba ujenzi wa hiki kituo ambacho nimekitaja Dege nimesema mapema Aprili, nataka nimthibitishie Mheshimiwa Mbunge kwamba kituo hiki mpaka ifikapo tarehe 30 mwezi wa Aprili kitakuwa kimeanza kufanya kazi. Pia alisema kwamba umeme katika kituo cha Kigamboni kinahudumia watu 12,000, nataka nimtaarifu kituo cha Mbagala pia kinahudumia wakazi wa Kigamboni na umeme mwingine ambao unatokea Ubungo. Ahsante sana.

Name

Suleiman Ahmed Saddiq

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mvomero

Primary Question

MHE. LUCY S. MAGERELI aliuliza:- Wilaya ya Kigamboni inakabiliwa na tatizo la msongo mdogo wa umeme na matukio ya kukatika umeme ya mara kwa mara hata mara tatu kwa siku:- Je, Serikali ina mpango gani wa kukomesha tatizo hilo?

Supplementary Question 2

MHE. SULEIMAN A. SADDIQ: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi. Naomba niulize swali dogo la nyongeza; kwa kuwa matatizo ya Wilaya ya Kigamboni yanafanana kabisa na matatizo ya Wilaya ya Mvomero; kwa kuwa katika Wilaya ya Mvomero, Kata ya Kibati kuna tatizo kubwa sana la msongo wa umeme na hivi ninapozungumza leo hapa Bungeni hakuna umeme Kibati kutokana na transfoma ya Kibati kuungua kwa zaidi ya mwezi mmoja sasa na wananchi wa Kibati wako gizani.

Je, Mheshimiwa Naibu Waziri yuko tayari kufanya ziara na mimi Kibati ili kuondoa tatizo hili ambalo wananchi wanateseka?

Name

Subira Khamis Mgalu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, naomba nijibu swali la Mheshimiwa Murad Saddiq, Mbunge wa Mvomero kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, kwanza tumepokea hiyo changamoto ambayo anasema katika Kata ya Kibati transfoma imeharibika, si tu kwamba inahitaji nifanye ziara bali inatakiwa wananchi hawa wapate huduma haraka, kwa hiyo naiagiza TANESCO Mkoa wa Morogoro suala la kuharibika kwa transformer halisubiri ziara, inatakiwa wafanye matengenezo haraka iwezekanavyo ili huduma iendelee.

Mheshimiwa Spika, hata hivyo, nataka nilisemee kwa ujumla; nimesema kwamba kuna matengenezo makubwa yanafanyika Mkoa wa Dar es Salaam kituo cha Ubungo ambacho kinapokea umeme kutoka Kidatu kwa njia ya msongo kilovoti 220 ambao unafika Morogoro unapoozwa unapelekwa Dar es Salaam. Kwa hiyo, matengenezo ya Dar es Salaam kwa kweli yana athari za moja kwa moja na upungufu wa Mkoa wa Morogoro, Mkoa wa Pwani na Mkoa wa Tanga; nichukue fursa hii kuwapa pole wakazi wa mikoa hii na kuwaomba radhi, lakini tuvumilie mwezi Aprili, mwaka huu 2019 yakikamilika matengenezo yale makubwa ambapo yamegharimu zaidi ya bilioni 32 hali itatulia.

Mheshimiwa Spika, ahsante sana.

Name

Joseph Michael Mkundi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ukerewe

Primary Question

MHE. LUCY S. MAGERELI aliuliza:- Wilaya ya Kigamboni inakabiliwa na tatizo la msongo mdogo wa umeme na matukio ya kukatika umeme ya mara kwa mara hata mara tatu kwa siku:- Je, Serikali ina mpango gani wa kukomesha tatizo hilo?

Supplementary Question 3

MHE. JOSEPH M. MKUNDI: Mheshimiwa Spika, nashukuru. Tatizo la kukatika kwa umeme limekuwa linajitokeza sana kwenye Visiwa vya Ukerewe hali inayoathiri shughuli za kiuchumi na hasa shughuli za utoaji wa huduma za afya kwenye hospitali yetu ya Wilaya ya Nansio.

Ningependa kupata kauli ya Serikali, ni mkakati gani uliopo kuondoa tatizo hili na kufanya Visiwa vya Ukerewe vipate umeme bila shida ya kukatikakatika kwa umeme kwenye maeneo hayo. Nashukuru sana.

Name

Subira Khamis Mgalu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kunipa fursa. Napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mkundi Mbunge wa Ukerewe kupitia Chama cha Mapinduzi kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba Mheshimiwa Mbunge aliwasilisha hilo leo asubuhi kwamba kuna tatizo hilo katika Visiwa vya Ukerewe na hapa nilipo nishatoa maelekezo kwamba kwa sababu umeme wa Ukerewe unatokea katika maeneo ya Bunda na kwa changamoto ambayo nimeipata hivi asubuhi baada ya kuwasiliana na Meneja kwamba kuna tatizo la changamoto ya nguzo, ndiyo maana Serikali imefanya maamuzi ya kuhama sasa itumie nguzo za zege.

Kwa hiyo, tumetoa maelekezo ifanyike utafiti wa kina changamoto ni nini ili ifanyiwe kazi, kwa hiyo namwomba Mheshimiwa Mbunge baada ya kutoka hapa tufanye mazungumzo ili kuweza kumpa mikakati ambayo Serikali imepanga. Ahsante.