Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 15 Sitting 2 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 13 2019-04-03

Name

Tauhida Cassian Gallos Nyimbo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. TAUHIDA CASSIAN GALLOS NYIMBO aliuliza:-

Je, Serikali ina mkakati gani juu ya raia wa kigeni wanaopewa vibali vya kuja kufanya kazi hapa nchini kwa muda na kuwazalisha watoto na wadogo zetu na inapofika muda wa kuondoka huwakimbia na kuwaacha watoto hao wakiishi maisha yao yote bila baba kitu ambacho huwasababishia unyonge katika maisha yao?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Tauhida Cassian Gallos, Mbunge wa Viti Maalum, Mkoa wa Magharibi, kama Ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi kupitia Idara ya Uhamiaji inatoa vibali vya ukaazi nchi kwa wageni baada ya Wizara ya Kazi kutoa vibali vya kazi kwa wageni hao.

Mheshimiwa Spika, mikakati ambayo Serikali inachukua ni kuelimisha raia wa Tanzania kuwa wasidhani kila mgeni anayekuja kufanya kazi Tanzania ni mtu mwema au ana uwezo wa kifedha na kutegemea kuwa atasaidiwa na mtoto wake kwenye malezi, hivyo kuwa waangalifu ili kuepuka madhara yanayoweza kutokea kutokana na kujiingiza kwao katika mahusiano ya kimapenzi na watu wasiowafahamu vema ikiwemo mimba na maradhi yanayosababishwa na ngono.