Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 15 Sitting 5 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 35 2019-04-08

Name

Zaynab Matitu Vulu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ZAYNABU M. VULU aliuliza:-

Barabara ya Vikindu – Vianzi hadi Sangatini ni muhimu kwa wakazi wa Jimbo la Mkuranga na Kigamboni:-

Je, ni lini barabara hiyo itajengwa kwa kiwango cha lami?

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. MWITA M. WAITARA) alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais - TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Zaynab Matitu Vulu, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, barabara ya Vikindu - Vianzi hadi Sangatini yenye urefu wa kilomita 18.65, inaanzia Kijiji cha Vikindu -Vianzi na Kitongoji cha Sangatini (Mkuranga) Mkoa wa Pwani na kuungana na barabara ya Kibada, Mwasonga hadi Tundisongani iliyopo Wilaya ya Kigamboni, Mkoa wa Dar es Salaam.

Mheshimiwa Naibu Spika, barabara hii kwa upande wa Wilaya ya Mkuranga inahudumiwa na Wakala wa Barabara za Vijiji na Mijini (TARURA) na kwa upande wa Wilaya ya Kigamboni inahudumiwa na Wakala wa Barabara nchini (TANROADS) Mkoa wa Dar es Salaam.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kutambua umuhimu wa barabara hii, TARURA Wilaya ya Mkuranga wameiomba Serikali shilingi milioni 270 katika bajeti ya mwaka wa fedha 2019/2020 za kuifanyia matengenezo maeneo korofi kwa urefu wa kilometa 18 na kujenga boksi kalvati moja lenye midomo miwili. Aidha, TARURA watafanya tathmini ya ujenzi kwa kiwango cha lami kipande wanachokisimamia na itakapokamilika, Serikali itazingatia matengenezo hayo kwa kutegemea na upatikanaji wa rasilimali fedha. Ahsante.