Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Zaynab Matitu Vulu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ZAYNABU M. VULU aliuliza:- Barabara ya Vikindu – Vianzi hadi Sangatini ni muhimu kwa wakazi wa Jimbo la Mkuranga na Kigamboni:- Je, ni lini barabara hiyo itajengwa kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 1

MHE. ZAYNABU M. VULU: Mheshimiwa Naibu Spika, asante sana. Kwa niaba ya wananchi wa Jimbo la Mkuranga na wanaotumia barabara hiyo, nina maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la kwanza, barabara hii ni muhimu sana kwa maendeleo ya wananchi wanozunguka eneo hilo; na kwa kuwa kuna haja ya kuiboresha; na kwa kuwa Serikali imesema wanasubiri TARURA wafanye tathmini ndiyo barabara hiyo ijengwe, je, hawaoni kwamba wakati wakifanya tathmini barabara hiyo iweze kutengenezwa angalau kwa kiwango cha kokoto?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, kwa kuwa barabara hii inaungana na barabara ya Kigamboni Mkoa wa Dar es Salaam ambayo iko TANROADS. Je, Serikali haioni sasa kuna haja ya barabara hii kuipandisha hadhi na kuiweka TANROADS ili iweze kupata huduma ambazo zinalingana na kule inapoishia ambapo inahudumiwa na TANROADS?

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. MWITA M. WAITARA): Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Naomba nijibu swali la Mbunge wa Viti Maalum, jirani yangu Mheshimiwa Zaynabu Vulu, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, swali lake la kwanza ni kwamba barabara hii inaweza ikapata matengenezo wakati tunasubiri mpango wa fedha ujao. Naomba niwaelekeze TARURA wa Wilaya hii ya Mkuranga wafanye utaratibu wa kukarabati maeneo korofi. Bahati nzuri katika mwaka huu wa fedha wametenga fedha shilingi milioni 270 ili zipelekwe katika eneo hili lakini tunaomba wafanye kazi hiyo mapema ili iendelee kupitika wakati wote na wananchi wasiendelee kupata shida katika eneo hili.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili ni kupandishwa hadhi kwa barabara hii. Suala la kupandishwa hadhi lina taratibu zake na mwongozo. Kwa hiyo, naomba Mheshimiwa Mbunge ashirikiane na Halmashauri yake wawasiliane na TANROADS, watafanya tathmini kama ikikidhi vigezo basi itakuwa ni vizuri ikapandishwa hadhi ili kupata huduma kubwa kidogo kulingana na mgao wa fedha ambao unatolewa. Ahsante.

Name

Mariamu Nassoro Kisangi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ZAYNABU M. VULU aliuliza:- Barabara ya Vikindu – Vianzi hadi Sangatini ni muhimu kwa wakazi wa Jimbo la Mkuranga na Kigamboni:- Je, ni lini barabara hiyo itajengwa kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 2

MHE. MARIAM N. KISANGI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kunipa nafasi ili nami niweze kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa tatizo kubwa la barabara hiyo ambayo inatoka Vianzi kwenda Marogoro mpaka Tundisongani ni daraja lililopo pale Tundisongani. Daraja hilo imekuwa ni shida mvua zinaponyesha wananchi wa Tundisongani na Wilaya ya Mkuranga wanakosa mawasiliano kabisa, hali ambayo imefanya Wabunge wa sehemu zote mbili Mkuranga na Kigamboni wamekaa pamoja lakini mpaka leo hakuna matunda yoyote juu ya barabara hii.

Je, Serikali sasa ina mpango gani wa kuboresha angalau lile daraja ili mvua zitakaponyesha wananchi wa Kigamboni na Mkuranga waweze kuwa na mawasiliano?

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. MWITA M. WAITARA): Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru, naomba nimjibu Mheshimiwa Mariam Kisangi, Mbunge wangu wa Mkoa wa Dar es Salaam kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa namna ambavyo ameuliza swali hili kwa uchungu na maeneo haya yote muhimu, kule Mkuranga kuna Naibu Waziri mwenzangu na kule Kigamboni Mheshimiwa Naibu Waziri wa Afya, naomba niwaelekeze TARURA, Mkoa wa Dar es Salaam walifanyie tathmini eneo hili na leo kabla ya saa saba nipate majibu nini kinaweza kufanyika ili kuondoa kero hii ya wananchi katika eneo hili. Ahsante.

Name

Dr. Raphael Masunga Chegeni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busega

Primary Question

MHE. ZAYNABU M. VULU aliuliza:- Barabara ya Vikindu – Vianzi hadi Sangatini ni muhimu kwa wakazi wa Jimbo la Mkuranga na Kigamboni:- Je, ni lini barabara hiyo itajengwa kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 3

MHE. DKT. RAPHAEL M. CHEGENI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, naomba na mimi awaelekeze TARURA ili washughulikie barabara ya kutoka Shigara kwenda Ruangwe. Kijiji cha Ruangwe ni Kisiwa katika Wilaya ya Busega. Naomba maelekezo ya Waziri yaende kwa TARURA vilevile.

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. MWITA M. WAITARA): Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Naomba niwaelekeze TARURA katika Wilaya ya Busega, watembelee maeneo yaliyotajwa na Mheshimiwa Mbunge Chegeni na wapate majibu ya kero hiyo ambayo ameitaja hapa Bungeni. Ahsante.

Name

Cosato David Chumi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafinga Mjini

Primary Question

MHE. ZAYNABU M. VULU aliuliza:- Barabara ya Vikindu – Vianzi hadi Sangatini ni muhimu kwa wakazi wa Jimbo la Mkuranga na Kigamboni:- Je, ni lini barabara hiyo itajengwa kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 4

MHE. COSATO D. CHUMI: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kuniona na kunipa nafasi. Pamoja na kazi nzuri wanayofanya TARURA Mkoa wa Iringa na katika Mji wa Mafinga, hali ya barabara za Mji wa Mafinga ambao ni kitovu cha shughuli za kiuchumi katika Wilaya ya Mufindi siyo ya kuridhisha, ni asilimia 24 tu ya baraba ambazo zinapitika kwa mwaka, ile tunaita good and fair. Je, Serikali ina mpango gani wa kuangalia Mji wa Mafinga kwa macho mawili ili kuhakikisha kwamba barabara za Mji wa Mafinga zinapitika kwa uzuri kwa mwaka mzima ili kusudi ku-speed up ukuaji wa uchumi ambao ndiyo kitovu cha Wilaya nzima ya Mufindi?

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. MWITA M. WAITARA): Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Naomba nimjibu Mheshimiwa Cosato Chimi, Mbunge wa Mafinga kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, mwanzo wa kuanzishwa TARURA ilikuwa ni kuondoa kero ambazo Waheshimiwa Wabunge wengi hapa wanazungumzia. Kwa hiyo, naomba niwaelekeze TARURA nchi nzima, wafanye tathmini ya kero kubwa na za muda mrefu katika maeneo yao. Tunatarajia kwenye bajeti ambayo tunakwenda kuijadili, maeneo haya ambayo yanazungumzwa na Waheshimiwa Wabunge, ndiyo maeneo ambayo yatakuwa yamezingatiwa kuondoa kero katika maeneo hayo kwa pamoja na eneo la Mafinga, TARURA kufanya kazi pale na Mkoa wa Iringa, naomba wataalam wetu, Mainjinia nchi nzima wa TARURA, wafanye tathmini na walete kero mahsusi ambazo Wabunge wamezungumza na Viongozi mbalimbali wamewasilisha ili ziondolewe katika maeneo hayo. Ahsante.