Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 15 Sitting 6 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 44 2019-04-09

Name

Justin Joseph Monko

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Singida Kaskazini

Primary Question

MHE. JUSTIN J. MONKO aliuliza:-

Tarafa ya Mtinko Jimbo la Singida Kaskazini yenye Kata sita haina kituo cha afya cha Serikali:-

(a) Je, Serikali ipo tayari kukamilisha jengo la kituo cha afya katika Kata ya Makuro lililojengwa na wananchi ili wananchi waweze kupata huduma za rufaa kutoka katika Zahanati zilizopo?

(b) Je, Serikali ipo tayari kutenga fedha za majengo ya ziada katika kituo cha afya Kata ya Makuro ili kutoa huduma bora kwa wananchi?

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. MWITA M. WAITARA) alijibu:-

Mheshimiwa Mnweyekiti, nakushukuru. Kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Justin Joseph Monko Mbunge wa Singida Kaskazini, lenye sehemu (a) na (b) kwa pamoja, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, Tarafa ya Mtinko yenye Kata sita ina zahanati tisa na haina kituo cha afya. Hata hivyo, wananchi wa Tarafa hiyo hupata huduma za afya za rufaa kwenye hospitali teule ya Wilaya ya St. Carols Council Designated Hospital.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika mwaka wa fedha 2018/2019, Halmashauri ya Singida imepokea jumla ya shilingi bilioni 2.6 kwa ajili ya ujenzi wa hospitali ya Wilaya na kukarabati vituo vya afya viwili yaani kituo cha afya cha Msange na kito cha afya cha Mgori ili kuweza kutoa huduma za upasuaji kwa mama na mtoto. Serikali itaendelea kujenga na kukamilisha maboma ya vituo vya kutolea huduma za afya kwa awamu kadri ya upatikanaji wa fedha utakavyowezeshwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kituo cha afya cha Makuro kimejengwa kwa nguvu za wananchi na mpaka sasa jengo la wagonjwa wa nje lipo katika hatua za ujenzi kwenye ukuta. Nazielekeza halmashauri kutenga fedha kwa ajili ya kukamilisha maboma na vituo vya kutolea huduma kwenye maeneo yao ya kiutawala. Serikali itaendelea kukamilisha maboma na kujenga kwa awamu kulingana na upatikanaji wa fedha. Ahsante.