Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Justin Joseph Monko

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Singida Kaskazini

Primary Question

MHE. JUSTIN J. MONKO aliuliza:- Tarafa ya Mtinko Jimbo la Singida Kaskazini yenye Kata sita haina kituo cha afya cha Serikali:- (a) Je, Serikali ipo tayari kukamilisha jengo la kituo cha afya katika Kata ya Makuro lililojengwa na wananchi ili wananchi waweze kupata huduma za rufaa kutoka katika Zahanati zilizopo? (b) Je, Serikali ipo tayari kutenga fedha za majengo ya ziada katika kituo cha afya Kata ya Makuro ili kutoa huduma bora kwa wananchi?

Supplementary Question 1

MHE. JUSTIN J. MONKO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa maswali ya kuuliza maswali madogo mawili ya nyongeza. Awali ya yote kwanza napenda niishukuru sana Serikali kwa fedha ambazo imetupatia sisi kwa ujenzi kama alivyoeleza Mheshimiwa Naibu Waziri. Hata hivyo, hospitali teule ya Wilaya ya Mtinko ambayo Mheshimiwa Naibu Waziri ameisema tangu ilipopandishwa hadhi mwaka jana haijapangiwa Madaktari wala Wauguzi wa kufanya kazi na kuongeza huduma katika hospitali hiyo. Je, Mheshimiwa Naibu Waziri yuko tayari kuwasiliana pia na Wizara ya Afya ili kuhakikisha kwamba hospitali hiyo inapata Wauguzi na Madaktari wa kutosha?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili; kwa kuwa Mheshimiwa Naibu Waziri anajua tofauti ya kituo cha afya na hospitali ya Wilaya na wananchi wale ambao ni zaidi ya wananchi 80,000 hawana kituo chochote cha afya na wamejenga jengo hilo kwa zaidi ya miaka nane na halmashauri yetu imeshindwa kutenga fedha za kukamilisha jengo hilo. Je, Wizara iko tayari kutenga fedha ya kukamilisha jengo hilo la kituo cha afya cha Makuro na kutenga fedha kwa ajili ya majengo mengine ili kituo cha afya cha Makuro kiweze kuanza kufanya kazi kwa Tarafa ya Mtinko. Ahsante?

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. MWITA M. WAITARA): Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwanza naomba nimpongeze Mheshimiwa Mbunge Monko kwa kuendelea kuwasimamia wananchi wa Jimbo lake la Singida Kaskazini. Sasa naomba nimjibu swali lake la kwanza na la pili kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la kwanza anazungumzia habari ya kupata Wauguzi na Madaktari. Naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge tumelipokea jambo hili, katika wale Wauguzi na Madaktari ambao tumewaomba kibali maalum Ofisi ya Utumishi wakipatikana, basi tutaangalia pia eneo hili ili wananchi waweze kupata huduma.

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili anazungumza habari ya kutenga fedha ya kukamilisha boma hili ambalo limejengwa kwa nguvu za wananchi. Namkaribisha Mheshimiwa Mbunge ofisini kwetu tuzungumze, tuone kitakachowezekana, lengo na makusudi ni kwamba jambo hili likamilike na nguvu za wananchi ziweze kuungwa mkono, zisipotee bure ahsante.

Name

Hawa Abdulrahiman Ghasia

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Mtwara Vijijini

Primary Question

MHE. JUSTIN J. MONKO aliuliza:- Tarafa ya Mtinko Jimbo la Singida Kaskazini yenye Kata sita haina kituo cha afya cha Serikali:- (a) Je, Serikali ipo tayari kukamilisha jengo la kituo cha afya katika Kata ya Makuro lililojengwa na wananchi ili wananchi waweze kupata huduma za rufaa kutoka katika Zahanati zilizopo? (b) Je, Serikali ipo tayari kutenga fedha za majengo ya ziada katika kituo cha afya Kata ya Makuro ili kutoa huduma bora kwa wananchi?

Supplementary Question 2

MHE. HAWA A. GHASIA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Kata ya Dihimba yenye vijiji zaidi ya 30 haina kituo cha afya hata kimoja na Kata ya Mangopachanne tayari wameshaanza ujenzi wa kituo cha afya. Je, Serikali iko tayari kuwaunga mkono katika kukamilisha kituo cha afya katika Kata ya Mangopachanne?

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. MWITA M. WAITARA): Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali hii ya Awamu ya Tano ya Chama cha Mapinduzi ipo tayari sana kuunga mkono wananchi hawa. Tuendelee kuwasiliana, tutatafuta fedha, zikipatikana tupeleke kukamilisha maboma yote na sio kule kwa Mheshimiwa Hawa Ghasia peke yake ila ni nchi nzima kwa Majimbo mbalimbali kukamilisha maboma yaliyojengwa na nguvu za wananchi.

Name

Flatei Gregory Massay

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Vijijini

Primary Question

MHE. JUSTIN J. MONKO aliuliza:- Tarafa ya Mtinko Jimbo la Singida Kaskazini yenye Kata sita haina kituo cha afya cha Serikali:- (a) Je, Serikali ipo tayari kukamilisha jengo la kituo cha afya katika Kata ya Makuro lililojengwa na wananchi ili wananchi waweze kupata huduma za rufaa kutoka katika Zahanati zilizopo? (b) Je, Serikali ipo tayari kutenga fedha za majengo ya ziada katika kituo cha afya Kata ya Makuro ili kutoa huduma bora kwa wananchi?

Supplementary Question 3

MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza. Jimbo la Mbulu Vijijini lina kituo kimoja tu cha afya, je wananchi wa Maretadu wamejenga sana kituo cha afya cha Maretadu, je, Mheshimiwa Waziriy uko tayari kutusaidia fedha ya kumalizia kituo cha afya Maretadu?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nimpongeza Naibu Waziri kwa majibu mazuri yote ya kwanza. Namfahamu Mheshimiwa Flatei Massay na katika Jimbo lake kulikuwa na changamoto kubwa sana ya afya na ndio maana katika kelele zake nyingi sana kwa kuwaombea wananchi wake tulimpelekea hospitali ya Wilaya na kituo cha afya cha Dongobeshi. Hata hivyo, tunalichukua ombi hilo tutalifanyia kazi kwa sababu lengo letu na mkakati wetu wananchi wote wapate huduma ya afya, kwa hiyo jambo hili tutalichukua, tutaangalia jinsi gani ya kulifanyia kazi.

Name

Alex Raphael Gashaza

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ngara

Primary Question

MHE. JUSTIN J. MONKO aliuliza:- Tarafa ya Mtinko Jimbo la Singida Kaskazini yenye Kata sita haina kituo cha afya cha Serikali:- (a) Je, Serikali ipo tayari kukamilisha jengo la kituo cha afya katika Kata ya Makuro lililojengwa na wananchi ili wananchi waweze kupata huduma za rufaa kutoka katika Zahanati zilizopo? (b) Je, Serikali ipo tayari kutenga fedha za majengo ya ziada katika kituo cha afya Kata ya Makuro ili kutoa huduma bora kwa wananchi?

Supplementary Question 4

MHE. ALEX R. GASHAZA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi ili niulize swali la nyongeza. Kwa kuwa ipo zahanati ya Kijiji cha Kigarama ambayo jengo la OPD limejengwa kwa nguvu ya wananchi mpaka kukamilika, lakini zahanati hiyo takribani miaka miwili haijaweza kufanya kazi kwa sababu hakuna nyumba ya watumishi na choo hakijakamilika. Upo uwezekano wa kupata nyumba ya kupanga kwenye center hiyo ya karibu ambapo ni rahisi Mganga kuweza kuhudumia akitokea hapo. Je, Wizara iko tayari kutoa kibali ili zahanati hiyo iweze kufunguliwa kuondoa adha ya akinamama wanaokwenda kujifungua kutembea umbali mrefu zaidi ya kilomita 30 wakati tayari wameshatoa mchango kwa ajili ya ujenzi wa zahanati hiyo?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza kwa kauli yako naomba nimwagize Mganga Mkuu wetu wa Mkoa wa Kagera aende akafanye ufuatiliaji wa zahanati hiyo, kama imekamilika kweli lazima wahakikishe nguvu za wananchi ambao lengo lao wapate huduma kuhakikisha kwamba wanaipata. Kwa hiyo namwagiza Mganga wetu Mkuu wa Mkoa wetu wa Kagera aende akafanye kazi ili na Mheshimiwa Mbunge apate kibali na wananachi wapate huduma.