Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 15 Sitting 8 Energy and Minerals Wizara ya Nishati 65 2019-04-11

Name

Silvestry Fransis Koka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibaha Mjini

Primary Question

MHE. SILVESTRY F. KOKA aliuliza:-

Mradi wa Umeme mkubwa wa msongo wa KVA 400 toka Kinyerezi kupitia Pwani, Morogoro, Singida na Arusha umechukua maeneo ya wananchi kwa muda mrefu bila kuwalipa fidia:-

Je, Serikali ina mpango gani sasa wa kulipa fidia hiyo?

Name

Subira Khamis Mgalu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya waziri wa Nishati, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Silyvestry Francis Koka, Mbunge wa Kibaha Mjini, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali kupitia TANESCO inatekeleza mradi wa kusafirisha umeme wa msongo wa Kilovolts 400 kutoa Kinyerezi - Dar es salaam na Rufiji - Pwani kupitia Chalinze hadi Dodoma. Malengo ya mradi huo ni kuongeza upatikanaji wa umeme katika ukanda wa Mashariki, Kati na kaskazini mwa nchi kutoka kwenye mitambo ya kuzalisha umeme (Kinyerezi) na mradi wa Rufiji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, awamu ya kwanza ya upimaji njia na kutathmini mali za wananchi watakaopisha mradi kutoka Kibaha hadi Chalinze ilikamilika Mwezi Desemba, 2017 na kuidhinishwa na Mthamini Mkuu wa Serikali Mwezi Novemba, 2018. Serikali kupitia TANESCO Mwezi Januari, 2019 itatangaza zabuni kwa ajili ya kumpata mtaalam mshauri wa kufanya upembuzi yakinifu wa ujenzi wa njia ya umeme wa msongo wa Kilovoti 400 kutoka Rufiji hadi Chalinze na kuhuisha upembuzi yakinifu wa njia ya umeme wa msongo wa kilovoti 400 kutoka Kinyerezi hadi Chalinze.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jumla ya shilingi bilioni 21 na milioni 600 zinatakiwa kulipwa kama fidia kwa wananchi katika maeneo ya Halmashauri za Kisarawe, Kibaha Mjini, Kibaha Vijijini na Chalinze na eneo la Kiluvya na taratibu zote za uandaaji taarifa na majedwali ya malipo ya fidia zimekamilika. Serikali inatarajia kutenga fedha kiasi cha shilingi bilioni 34 kupitia bajeti ya mwaka wa fedha 2019/2020 kwa ajili ya malipo ya fidia kwa wananchi wa maeneo hayo baada ya kukamilika kazi ya kuhuisha upembuzi yakinifu ikiwa ni pamoja na gharama za mradi wa kipande cha Kinyerezi Chalinze.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunaomba wananchi waendelee kuvuta subira wakati Serikali inaendelea kukamilisha taratibu za malipo yao ya fidia. Ahsante.