Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 3 Sitting 14 Public Service Management Ofisi ya Rais TAMISEMI. 111 2016-05-06

Name

Doto Mashaka Biteko

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukombe

Primary Question

MHE. DOTO M. BITEKO aliuliza:-
Je, kwa nini Serikali inachukua muda mrefu sana kurekebisha mishahara ya Walimu baada ya kupandishwa vyeo?

Name

Angellah Jasmine Mbelwa Kairuki

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nominated

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Doto Mashaka Biteko, Mbunge wa Bukombe, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kwamba miaka ya nyuma kulikuwepo na ucheleweshaji wa kurekebisha mishahara kwa kuwa mfumo wa taarifa za kiutumishi na mishahara wa wakati huo ulimtaka kila Mwajiri kuwasilisha marekebisho ya Watumishi wake Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuanzia mwaka 2012 Mfumo huu wa Taarifa za Kiutumishi na Mishahara uliimarishwa kutoka Toleo la 7 kwenda Toleo la 9 la Lawson ambapo mwajiri alisogezewa huduma ya kufanya marekebisho mbalimbali ya kiutumishi yanayotokea katika ofisi yake bila ya kulazimika kusafiri kwenda Dar es Salaam. Utaratibu huu umekuwa na manufaa ambapo kwa sasa mabadiliko mbalimbali ya kiutumishi yanafanywa na mwajiri kwa kuzingatia mzunguko wa malipo ya mishahara kwa kila mwezi.
Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na utaratibu huu mzuri, mazingira machache yanayoweza kuchelewesha marekebisho ya mishahara kufanyika kwa wakati, kutokana na kuingizwa kwa taarifa za watumishi kwenye mfumo baada ya orodha ya malipo ya mishahara katika mwezi husika kufungwa, au waajiri kufanya mabadiliko bila ya kuweka taarifa muhimu hususan viambatisho kama vile barua za kupandishwa cheo na taarifa kutumwa, zikiwa na makosa.
Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kupitia Bunge lako Tukufu, kuwataka waajiri wote kufanya marekebisho ya mishahara kwa watumishi wote kwa wakati kama ambavyo imekuwa ikielekezwa na Serikali ili kuepusha ucheleweshaji wa haki za watumishi.