Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Doto Mashaka Biteko

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukombe

Primary Question

MHE. DOTO M. BITEKO aliuliza:- Je, kwa nini Serikali inachukua muda mrefu sana kurekebisha mishahara ya Walimu baada ya kupandishwa vyeo?

Supplementary Question 1

MHE. DOTO M. BITEKO: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nimshukuru Mheshimiwa Waziri kwa majibu yake, vilevile niwashukuru sana ndugu Thadei Mushi kwa naMheshimiwa Naibu Spika, nina maswali mawili madogo ya nyongeza; kwa kuwa Serikali inafahamu baada ya kuwa imempandisha daraja Mwalimu na kumrekebishia mshahara inachukua muda mrefu sana. Utumishi hawaoni kuwa nao imefika wakati wachukue ile model wanayochukua watu wa Nishati na Madini ijulikane kabisa kwamba ukipandishwa daraja kwa kipindi fulani mshahara wako utakuwa umerekebishwa ili watumishi hawa wawe na uhakika?
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, kwa kuwa malimbikizo ya mshahara baada ya kurekebishwa mshahara yanachukua muda mrefu, Serikali inawaambia nini watumishi wa umma hususan Walimu kwamba watalipwa lini, kwa uharaka zaidi malimbikizo ya mshahara haya ambayo yanachukua miaka mingi sana kabla ya kulipa?mna wanavyotupa ushirikiano.

Name

Angellah Jasmine Mbelwa Kairuki

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nominated

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI NA UTAWALA BORA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Kwanza kabisa nimshukuru kwa namna ambavyo amekuwa akifuatilia sana masuala mazima ya ustawi na maslahi ya utumishi wa umma hususan Walimu. Natambua ametokana na Chama cha Waalimu Tanzania, nakupongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Biteko alitaka kufahamu endapo Serikali labda kwa nini isifikirie mtumishi anapopandishwa daraja moja kwa moja aweze kuwa amefanyiwa marekebisho yake.
Mheshimiwa Naibu Spika, kama ambavyo nilieleza kinachofanyika kupitia Mfumo huu wa Taarifa za Kiutumishi na nashukuru kwamba ameweza kumpongeza Afisa Utumishi aliyeko katika Wilaya ya Bukombe kwa kazi nzuri anayoifanya, wanapokuwa Kamati ya Ajira imeshampatia barua ya kupandishwa cheo, kinachofanyika wana-post katika mfumo huu wa Lawson wa taarifa za kiutumishi na mishahara, lakini ni jukumu sasa la Utumishi kuhakikisha kwamba, mtumishi huyu aliyepandishwa cheo kwanza taarifa zake za tathmini kwa uwazi kwenye OPRAS zipo, kuhakikisha kwamba katika muundo wa utumishi kweli anastahili kupanda katika ngazi hiyo na kutokana na sifa na uzoefu ambao umeainishwa katika muundo wa maendeleo ya utumishi.
Mheshimiwa Naibu Spika, vile vile kuhakikisha kwamba ni kweli ana utendaji mzuri pamoja na uadilifu. Bado naendelea kuhimiza niwaombe sana waajiri pamoja na Maafisa Utumishi ambao wanasimamia suala zima la mfumo huu, kuhakikisha kwamba wanapandisha kwa wakati vilevile wanafanya marekebisho kwa wakati kwa kuzingatia maelekezo mbalimbali ambayo tumewapatia.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa upande wa madeni ya Walimu napenda tu kusema kwamba kwa kiasi kikubwa madeni haya yamelipwa, zaidi ya Walimu 13,000 tayari malimbikizo yao wameshalipwa ya mishahara, vilevile kwa upande wa Hazina madeni mbalimbali yamekuwa yakilipwa. Bado naendelea kusisitiza tena kuhakikisha kwamba, waajiri wanalipa kwa wakati malipo haya na kuhakikisha kwamba wanayatengea bajeti katika mwaka husika, vile vile wapandishe watumishi kwa kuzingatia muundo na kwa kuzingatia kwamba wana Ikama hiyo na bajeti kwa sababu wasipofanya hivyo ndiyo maana wanasababisha malimbikizo mbalimbali.
Mheshimiwa Naibu Spika, vilevile changamoto nyingine ambayo tumekuwa tikiipata, unakuta mfumo wetu wa Lawson una-calculate automatic arrears, wakati huo huo unakuta Mwajiri mwingine naye analeta manual arrears, kwa hiyo tusipokuwa makini kufanya uhakiki unaweza ukajikuta umemlipa mtumishi mmoja malipo ambayo hayastahiki. Bado naendelea kusisitiza kwamba, Serikali inatambua umuhimu wa watumishi na itakuwa ikiendelea kulipa kila mara kwa kadri ambavyo uwezo umekuwa ukiruhusu.