Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 15 Sitting 12 Water and Irrigation Wizara ya Maji 105 2019-04-17

Name

Willy Qulwi Qambalo

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Karatu

Primary Question

MHE. QAMBALO W. QULWI aliuliza:-

Kijiji cha Makhoromba ni kati ya vijiji 10 vilivyopangwa kunufaika katika mpango wa WSDP-I Wilayani Karatu. Hadi hivi sasa Wilayani Karatu mradi wa maji katika kijiji hicho haujatekelezwa:-

Je, ni lini Serikali itatekeleza mradi huo ili wananchi hao waondokane na tatizo kubwa la kukosa huduma ya maji?

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Maji, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Qambalo Willy Qulwi, Mbunge wa Karatu, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, Kijiji cha Makhoromba kina vitongoji vinne na kwa sasa upo mradi uliotekelezwa na Hifadhi ya Taifa ya Ngorongoro kwa kushirikiana na wananchi pamoja na Halmashauri ya Wilaya ya Karatu, ambao unatoa huduma katika vituo vitatu vya kuchotea maji, lakini kutokana na ugumu wa kijiografia haukuweza kufika kila kitongoji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuona umuhimu wa kutatua tatizo la uhaba wa maji katika maeneo mengi ya kijiji hicho, Serikali iliweka kijiji hicho kuwa miongoni mwa vijiji 10 vilivyopangwa kunufaika na programu ya WSDP-I. Aidha, mradi wa maji katika kijiji hicho haukutekelezwa kwa kuwa kipaumbele kiliwekwa katika ukamilishaji wa miradi mingine ya WSDP-I iliyokuwa imeanza kutekelezwa kabla ya kluanzisha miradi mipya.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imeelekeza Halmashauri ya Wilaya ya Karatu kutafuta vyanzo vya uhakika vyenye maji ya kutosha vitakavyoweza kuhudumia maeneo mengi ya kijiji hicho kulingana na jiografia yake na kufanya usanifu wa mradi huo utengewe fedha katika mwaka wa 2019/2020.