Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 15 Sitting 15 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 128 2019-04-24

Name

Mattar Ali Salum

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Shaurimoyo

Primary Question

MHE. MATTAR ALI SALUM aliuliza:-

Jeshi la Polisi lipo kwa mujibu wa sheria na hupaswa kufanya kazi kwa mujibu wa sheria za nchi. Jeshi la Polisi linapowakamata baadhi ya watu huamuru wawekwe ndani zaidi ya saa 24 na kusababisha usumbufu mkubwa:-

Je, ni kesi zipi mtuhumiwa anapaswa kuwekwa ndani chini ya saa 24.

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mattar Ali Salum, Mbunge wa Shaurimoyo, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, makosa yote isipokuwa yaliyoainishwa katika kifungu 148(5)(a)-(e) cha Sheria ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai, Sura ya 20 yana dhamana. Watuhumiwa wake hawapaswi kukaa mahabusu zaidi ya saa 24. Aidha, watuhumiwa ambao wanakaa ndani zaidi ya saa 24 ilhali makosa yao yana dhamana hutokana na sababu kwamba watuhumiwa hao wameshindwa kutimiza masharti na vigezo vya kupata dhamana kwa mujibu wa Sheria ya Mwenendo wa Makosa la Jinai Kifungu cha 65 na 66, Sura ya 20 kama ambavyo imefanyiwa mapitio mwaka 2002.