Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Mattar Ali Salum

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Shaurimoyo

Primary Question

MHE. MATTAR ALI SALUM aliuliza:- Jeshi la Polisi lipo kwa mujibu wa sheria na hupaswa kufanya kazi kwa mujibu wa sheria za nchi. Jeshi la Polisi linapowakamata baadhi ya watu huamuru wawekwe ndani zaidi ya saa 24 na kusababisha usumbufu mkubwa:- Je, ni kesi zipi mtuhumiwa anapaswa kuwekwa ndani chini ya saa 24.

Supplementary Question 1

MHE. MATTAR ALI SALUM: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Swali la kwanza, kuna askari ambao wanawaweka ndani wananchi wetu bila ya kuwa na makosa ya kuwekwa ndani. Vilevile, wengine wanawaweka ndani zaidi ya saa 24 wakiwa hawana makosa ya kuwekwa ndani saa 24. Je, Wizara yako inatoa kauli gani juu ya Maaskari hawa kuhakikisha wanaepuka kuwaweka ndani wananchi wetu zaidi ya saa 24?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, Watanzania wengi hawana elimu ya sheria hii ya Jeshi la Polisi. Je, Serikali ina mikakati gani ya kutoa elimu kwa wananchi wetu ili waweze kujua haki zao za msingi? Ahsante.

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Mattar, Mbunge wa Shaurimoyo, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika jibu langu la msingi nilieleza kwamba ukiachilia mbali Kifungu 148(5) ambacho kimeainisha makosa ambayo hayana dhamana, lakini kuna Kifungu cha 65 pamoja na 66 vya sheria hiyo hiyo ambayo vinaeleza ni kwa jinsi gani hayo makosa ambayo yana dhamana itatolewa kwa utaratibu upi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mfano, Kifungu cha 65 kinaeleza umuhimu wa kufahamu historia na familia ya mhusika lakini kifungu cha 66 kinaeleza kwamba mtuhumiwa huyu ambaye anaomba dhamana anatakiwa aweze kuandika kwa mkono wake kwamba atarudi siku ya kesi yake itakapokuwa imeitwa. Kwa hiyo, pamoja na mambo mengine, dhamira kubwa ni kuona jinsi gani mtu huyu anapoachiwa kwenda nje hawezi kuwa hatari kwa usalama wake mwenyewe ama kwa jamii ambayo inamzunguka. Kwa hiyo, inawezekana labda wananchi wanashindwa kufahamu kwamba Polisi wanapomweka mtu zaidi ya saa 24 wakati makosa yana dhamana kwamba kuna mambo ambayo masharti yake hayajatimizwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, nitutoe wito kwa wananchi kuweza kutumia fursa ya Jeshi letu la Polisi pamoja na Serikali kwa ujumla tunapoweza kuzungumza mara kwa mara kuwaelimisha ili wafahamu sheria za nchi yetu na wafahamu haki zao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia ni jukumu la Wabunge kuweza kuwaelimisha wananchi wetu ikiwemo Mheshimiwa Mattar kupitia mikutano yake mbalimbali katika jimbo lake…

MWENYEKITI: Ahsante.

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: …atumie fursa hiyo kuweza kuwawezesha wananchi kufahamu sheria za nchi hii ili waweze kuepuka madhara…

MWENYEKITI: Haya, ahsante sana Mheshimiwa Waziri. Mheshimiwa Selasini.

Name

Joseph Roman Selasini

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Rombo

Primary Question

MHE. MATTAR ALI SALUM aliuliza:- Jeshi la Polisi lipo kwa mujibu wa sheria na hupaswa kufanya kazi kwa mujibu wa sheria za nchi. Jeshi la Polisi linapowakamata baadhi ya watu huamuru wawekwe ndani zaidi ya saa 24 na kusababisha usumbufu mkubwa:- Je, ni kesi zipi mtuhumiwa anapaswa kuwekwa ndani chini ya saa 24.

Supplementary Question 2

MHE. JOSEPH R. SELASINI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana. Waziri wa Mambo ya Ndani alitoa maelekezo mazuri sana kwa trafiki juu ya matumizi ya tochi za barabarani, kutopiga kamera gari kwa nyuma na kurusha picha kwa wenzao mbele ya safari. Lakini mtindo huu unaendelea na juzi siku ya Ijumaa Kuu walimkamata Diwani wangu wakampeleka polisi pale Himo…

MWENYEKITI: Swali, swali Mheshimiwa.

MHE. JOSEPH R. SELASINI: …na kum-harass sana. Sasa je, Waziri uko tayari kufafanua hayo maelekezo ili yaweze kutumika vizuri wananchi waache kusumbuliwa?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, hii hoja ya maelekezo ya Mheshimiwa Waziri ambaye ndiyo mwenye dhamana ya mwisho katika Wizara yetu na vyombo ambavyo anavisimamia inapaswa itekelezwe na tulitolea ufafanuzi vizuri katika kongamano ambalo tulifanya juzi la usalama barabarani, watu walileta hoja mbalimbali kuhusiana na umuhimu wa kutokuitekeleza hoja ile.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini tulikuwa tuna vigezo na hoja za msingi za kusimamia maamuzi ya Mheshimiwa Waziri. Kwa hiyo, nisisitize kwamba askari wote nchi nzima waendelee kutii na kufuata maelekezo ambayo tunayatoa kama Wizara. Na sisi tutaendelea kutoa ufafanuzi pale ambapo tutapata fursa.