Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 15 Sitting 15 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 129 2019-04-24

Name

Machano Othman Said

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

House of Representatives

Primary Question

MHE. MACHANO OTHMAN SAID aliuliza:-

(a) Je, ni Wizara ipi inayo wajibika kukusanya fedha za Viza na kusimamia utoaji wa Viza hizo?

(b) Je, kuna mgao wowote kwenda Serikali ya Mapinduzi Zanzibar kupitia uwanja wake wa ndege wa Kimataifa wa Abeid Karume?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Machano Othman Said, Mbunge wa Baraza la Wawakilishi lenye sehemu (a) na (b) yote kwa pamoja kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi kupitia Idara ya Uhamiaji ndiyo inayowajibika kukusanya fedha za Viza na kusimamia utoaji wa Viza. Aidha, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kupitia Balozi za Tanzania ndiyo inayo kusanya fedha za Viza na kusimamia utoaji wa Viza katika Balozi zetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, makusanyo yote ambayo yanayokusanywa na Idara ya Uhamiaji Zanzibar kupitia vyanzo vya mapato ikiwemo mapato yatokanayo na Viza kupitia uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Abeid Amani Karume huwasilishwa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.