Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 15 Sitting 30 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 245 2019-05-17

Name

Omar Abdallah Kigoda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Handeni Mjini

Primary Question

MHE. OMARI A. KIGODA aliuliza:-

Hospitali ya Handeni inahudumia karibu Majimbo manne lakini ina upungufu wa vifaa ambao unasababisha wagonjwa wengi kupewa rufaa:-

Je, Serikali haioni umuhimu wa kuongeza vifaa ili watu wengi wapate huduma?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE) alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais –TAMISEMI naomba kujibu swali la Mheshimiwa Omari Abdallah Kigoda, Mbunge wa Handeni kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika kuhakikisha wananchi wanapata huduma inayofaa katika Hospitali ya Mji Handeni kwa kipindi cha mwaka wa fedha 2016/2017 na 2017/2018 Serikali imeongeza vifaa tiba muhimu ambavyo ni; ultra sound, urine chemistry analyzer, gene expert machine na cryotherapy machine. Serikali imeendelea kuongeza bajeti ya vifaa tiba kila mwaka na katika mwaka wa fedha 2019/ 2020 fedha zitakazotumika kununua vifaa tiba katika Hospitali ya Handeni ni shilingi milioni 96 ikiwa ni ongezeko la shilingi milioni 20 ikilinganishwa na bajeti ya vifaa tiba kwa mwaka wa fedha 2018/2019.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kutambua umuhimu wa kuondoa msongamano kwenye Hospitali ya Halmashauri ya Mji Handeni, Serikali katika mwaka wa fedha 2019/2020 imetenga kiasi cha shilingi milioni 500 kwa ajili ya kuanza ujenzi wa Hospitali ya Halmashauri ya Handeni. Aidha, kwa mwaka wa fedha 2017/2018 na 2018/2019 Serikali ilitoa kiasi cha shilingi milioni 800 kwa ajili ya ukarabati na upanuzi wa Vituo vya Afya vya Kabuku na Mkata vilivyopo katika Halmashauri ya Wilaya ya Handeni sambamba na ununuzi wa vifaa tiba vyenye thamani ya shilingi milioni 300 ili kuviwezesha vituo hivyo kutoa huduma bora. Serikali inazielekeza halmashauri kuendelea kutenga fedha kwenye bajeti zake kwa ajili ya ununuzi na ukarabati wa vifaa tiba.