Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Omar Abdallah Kigoda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Handeni Mjini

Primary Question

MHE. OMARI A. KIGODA aliuliza:- Hospitali ya Handeni inahudumia karibu Majimbo manne lakini ina upungufu wa vifaa ambao unasababisha wagonjwa wengi kupewa rufaa:- Je, Serikali haioni umuhimu wa kuongeza vifaa ili watu wengi wapate huduma?

Supplementary Question 1

MHE. OMARI A. KIGODA: Mheshimiwa Mwenyekiti, asante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza Bunge lililopita niliuliza kuhusu suala la ambulance na Mheshimiwa Waziri aliniambia tuendelee kutumia magari ya kawaida mpaka ambulance itakapopatikana. Tatizo la magari ya kawaida hayana vifaa maalum vya huduma ya kwanza kwa hiyo wagonjwa wengi wanaotoka pale hospitali kwenda hospitali nyingine wengi wanapoteza maisha njiani. Sasa nauliza tena, je, ni lini tena Serikali itaona umuhimu wa kuipatia Hospitali ya Handeni ambulance, asante sana.

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba uniruhusu kipekee kabisa nitumie fursa hii kuwapongeza Wabunge wa Mkoa wa Tanga maana maswali ya kuhusiana na afya wiki hii yamekuwa kila leo yakiulizwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika swali lake ambalo anauliza juu ya umuhimu wa Serikali kuhakikisha kwamba inapatikana ambulance kama ambavyo tulishawahi kujibu hapa, naomba niendelee kumsihi Mheshimiwa Mbunge kwamba Serikali kwa kupitia Wizara ya Afya ipo kwenye mchakato katika hatua za mwisho kuhakikisha kwamba ambulance zinanunuliwa. Na naamini katika maeneo ambayo yatakumbukwa kuhakikisha kwamba kile tulichoahidi kama Serikali tunatekeleza na yeye atapata.

Name

Joram Ismael Hongoli

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lupembe

Primary Question

MHE. OMARI A. KIGODA aliuliza:- Hospitali ya Handeni inahudumia karibu Majimbo manne lakini ina upungufu wa vifaa ambao unasababisha wagonjwa wengi kupewa rufaa:- Je, Serikali haioni umuhimu wa kuongeza vifaa ili watu wengi wapate huduma?

Supplementary Question 2

MHE. JORAM I. HONGOLI: Mheshimiwa Mwenyekiti, asante sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Jimbo la Lupembe Halmashauri ya Wilaya ya Njombe ina vituo vinne na kimoja kipo kwenye ujenzi lakini vituo vyote hivi havina vifaa muhimu kama vile Ultra sound na X-ray machines pamoja na kwamba tunatoa huduma ya upasuaji katika Kituo cha Lupembe.

Je, ni lini Serikali italeta vifaa hivi muhimu sana kwa ajili ya kuwasaidia wananchi waweze kupima baadhi ya vipimo kwenye hivi vituo vya afya? Ahsante sana.

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Hongoli, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, nikiri kabisa, kama kuna Wabunge ambao wanafuatilia masuala ya afya kwenye majimbo yao, ni pamoja na Mheshimiwa Hongoli na hivi karibuni alikuja ofisini na tukakubaliana. Amepata fursa ya Kituo cha Afya cha Kichiwa kinajengwa na naomba uniruhusu, ifike mahali nitaleta orodha ya jinsi ambavyo Serikali imefanya commitment na fedha ambazo tumeshalipa MSD, kinachosubiriwa ni vifaa kupelekwa. Kama ambavyo nimekuwa nikijibu kwamba ni azma ya Serikali kuhakikisha vituo vya afya vyote ambavyo vinajengwa vinapatiwa vifaa ili vitumike kama ambavyo tumekusudia.

Name

Raphael Michael Japhary

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Moshi Mjini

Primary Question

MHE. OMARI A. KIGODA aliuliza:- Hospitali ya Handeni inahudumia karibu Majimbo manne lakini ina upungufu wa vifaa ambao unasababisha wagonjwa wengi kupewa rufaa:- Je, Serikali haioni umuhimu wa kuongeza vifaa ili watu wengi wapate huduma?

Supplementary Question 3

MHE. RAPHAEL J. MICHAEL: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa nafasi ya swali la nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Manispaa ya Moshi ilishaleta ombi Serikali Kuu la muda mrefu kidogo, zaidi ya miaka minne, mitano, kuomba kupandishwa hadhi kwa Zahanati za Kata za Longuo, Ng’ambo na Msaranga, lakini bahati mbaya mpaka leo Serikali haijatujibu na tuna tatizo la huduma ya miundombinu ya afya katika Manispaa ya Moshi kwa sababu hatuna hospitali ya wilaya na hospitali ya wilaya Serikali haikuwa tayari kutukubalia ombi letu. Je, ni lini hadhi ya vituo hivyo itapandishwa ili tuwe na vituo vya afya vya kutosha?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nijibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Raphael Japhary Michael, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza, uwepo wa zahanati umuhimu wake hauondoki kwa kuondoa zahanati kuifanya eti kituo cha afya, kwa hiyo msimamo wa Serikali kwanza ni suala la uwepo wa zahanati lakini pia na uwepo wa vituo vya afya. Pale ambapo inaonekana kwamba hakuna namna, baada ya kujiridhisha kwamba matakwa yote ya kutoka zahanati kwenda kituo cha afya, hapo ndipo Serikali tunafanya kupandisha.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo sio rahisi kwa swali ambalo Mheshimiwa Mbunge ameuliza bila kujiridhisha kwamba yale matakwa ya kituo cha afya ambayo ni tofauti na zahanati yametimizwa. Inawezekana ndiyo maana na yeye mwenyewe anaridhika kwamba Serikali tunahakikisha tunajenga vituo vya afya tukizingatia ramani lakini pia na eneo ambalo zahanati zinatakiwa kuwepo na vituo vya afya vinatakiwa kuwepo.

Name

Kunti Yusuph Majala

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. OMARI A. KIGODA aliuliza:- Hospitali ya Handeni inahudumia karibu Majimbo manne lakini ina upungufu wa vifaa ambao unasababisha wagonjwa wengi kupewa rufaa:- Je, Serikali haioni umuhimu wa kuongeza vifaa ili watu wengi wapate huduma?

Supplementary Question 4

MHE. KUNTI Y. MAJALA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Kituo cha Afya cha Hamai kilichopo Wilayani Chemba kina upungufu mkubwa wa vifaatiba. Kituo hicho ndicho kinachotumika kama hospitali ya wilaya, kinahudumia wananchi wote wa Jimbo la Chemba, lakini pili, majirani zetu kwa maana ya Chilonwa na Jimbo la Kiteto mpakani kule. Sasa nataka kujua Wizara imejipangaje kutupatia vifaatiba zikiwemo x-ray machines pamoja na ultrasound? La pili suala zima la ambulance yetu, imechoka haitamaniki, haithamaniki. Nataka kupata majibu ya Waziri kuhusiana na hicho kituo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru.

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nijibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Kunti, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama ambavyo nimejibu katika jibu lililotangulia, kwamba ni azma ya Serikali kuhakikisha kwamba vituo vyote vya afya vinapelekewa vifaa. Niruhusu nichukue fursa hii kuiagiza MSD kuhakikisha kwamba zile oda zote ambazo zimepelekwa kuwe na msukumo wa kuhakikisha kwamba hivyo vifaa vinapatikana mapema ili viweze kutumika katika vituo vya afya kama Serikali tulivyokusudia. Pia ni ukweli usiopingika kwamba MSD safari hii wanakwenda kuagiza kutoka kwa manufacturer, sio habari ya kuagiza kutoka kwa mtu wa kati na kuna specifications ambazo lazima tuzingatie, lakini ni vizuri tukahakikisha jambo hili linafanyika mapema.