Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 15 Sitting 30 Justice and Constitutional Affairs Wizara ya Katiba na Sheria 250 2019-05-17

Name

Dr. Ally Yusuf Suleiman

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Mgogoni

Primary Question

MHE. DKT. SULEIMAN ALLY YUSSUF aliuliza:-

Ibara ya 130 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano inataja kazi za Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora, moja ya kazi zake ni kufanya uchunguzi juu ya mambo yanayohusu uvunjaji wa Haki za za Binadamu na ukiukwaji wa msingi ya utwala bora.

(a) Je, kwa nini ripoti za tume hiyo haziwekwi wazi kwa Umma?

(b) Je, Serikali haioni kuwa umefika wakati wa kujenga utamaduni wa ripoti hizo kujadiliwa Bungeni?

Name

Dr. Augustine Philip Mahiga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nominated

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA (K.n.y. WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA) alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Katiba na Sheria napenda kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. Suleiman Ally Yussuf Mbunge wa Mgogoni lenye sehemu (a) na (b) kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kabla sijalijibu Mheshimiwa Ally Yussuf, amesema wadhurumiwa wote kwa hiyo inawezekana hata yeye kuna ambao amewadhurumu lakini naomba nijibu swali kama alivyouliza maana hakuuliza hivyo huko nyuma.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kweli kwamba Ibara ya 130 ya katiba ya Jamhuri ya Muugano ikiosomwa kwa pamoja na sheria ya Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora Na. 7 ya 2001) inaipa Tume mamlaka ya kufanya uchunguzi wa mambo yote yanayohusu uvunjwaji wa haki za binadamu, kifungu cha 28(1)(a) mpaka (f) cha sheria hiyo (Na. 7 ya 2001) kinafafanua kuwa, tume baada ya kufanya uchunguzi na kuthibitisha kuwepo kwa uvunjifu wa haki za binadamu itawaslisha taarifa na mapendekezo yake kwenye mamlaka kusika kwa ajili ya utekelezaji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kifungu cha 33 (1) (a) –(c) cha Sheria Na. 7 ya 2001 kinaitaka Tume kuwasilisha taarifa yake ya mwaka katika Bunge la Jamhuri ya Muungano na Baraza la Mawaziri kupitia wanaoshughulikia masuala ya haki za binadamu kwa Tanzania Bara na Zanzabar, hata hivyo, Tume imekuwa ikitimiza jukuu hilo kwa mujibu wa sheria. Aidha, hakuna sheria yoyote inayokataza taarifa za Tume kujadiliwa Bungeni endapo Mbunge ataona kama kuna jambo la kuibua kutoka kwenye taarifa iliyowasilishwa.