Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 3 Sitting 29 Health and Social Welfare Ofisi ya Rais TAMISEMI. 239 2016-05-26

Name

Selemani Moshi Kakoso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpanda Vijijini

Primary Question

MHE. MOSHI S. KAKOSO aliuliza:-
Hospitali ya Wilaya ya Mpanda ndiyo pekee inayotoa huduma za Mkoa katika Mkoa wa Katavi, kwa kutumia bajeti ya Halmashauri ya Wilaya ya Mpanda;
Je, ni lini Hospitali ya Mkoa itajengwa?

Name

George Boniface Simbachawene

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibakwe

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS (TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA) alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Moshi Suleiman Kakoso Mbunge wa Mpanda Vijijini kama ifuatavyo:
Mheshimiwa Naibu Spika, taratibu za awali za ujenzi wa hospitali ya Mkoa wa Katavi zimeshaanza ambapo eneo la ekari 243 limepatikana. Katika bajeti ya mwaka 2014/2015, Mkoa ulipokea shilingi milioni 750, kati ya hizo shilingi milioni 468 zilitumika kulipa fidia kwa wananchi walioachia maeneo yao kupisha ujenzi wa hospitali. Hadi sasa Mkoa upo katika hatua za mwisho kusaini mkataba na kampuni ya Y and P Consultant ikiwa ni hatua muhimu ya kuanza ujenzi.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika bajeti ya mwaka 2016/2017, Serikali imetenga shilingi bilioni 1.4 ili kuendelea na ujenzi wa hospitali ya Mkoa katika Mkoa mpya wa Katavi.