Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Selemani Moshi Kakoso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpanda Vijijini

Primary Question

MHE. MOSHI S. KAKOSO aliuliza:- Hospitali ya Wilaya ya Mpanda ndiyo pekee inayotoa huduma za Mkoa katika Mkoa wa Katavi, kwa kutumia bajeti ya Halmashauri ya Wilaya ya Mpanda; Je, ni lini Hospitali ya Mkoa itajengwa?

Supplementary Question 1

MHE. MOSHI S. KAKOSO: Mheshimiwa Naibu Spika, ninashukuru kwa majibu ambayo Serikali imetoa ya hatua ya awali ya ujenzi wa hospitali ya Mkoa.
Swali langu la msingi nimeuliza kwa kuwa, hospitali ya Halmashauri ya Wilaya ya Mpanda ndiyo iliyobeba uzito wa kuhudumia takribani wagonjwa zaidi ya laki tano wanaotumia bajeti ya Halmashauti ya Wilaya ya Mpanda, ni lini Serikali itaharakisha mchakato wa ujenzi huo wa hospitali ya Mkoa ili kuepusha Halmashauri ya Mpanda inayotumia bajeti ya Halmashauri kwa ajili ya kuhudumia wagonjwa wengi kinyume na utaratibu.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujua Serikali ina mpango gani wa dharura wa kuisaidia hospitali hii ili iweze kukidhi mahitaji kwa sasa?
Lakini swali la piliā€¦
MHE. MOSHI S. KAKOSO: Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili naomba kuweka uzito, tunavyo vituo vya afya ambavyo kama vingeimarishwa vingesaidia sana uzito wa hii hospitali ambayo imeelemewa. Serikali ina mpango gani wa kuviboresha vituo vya afya ambavyo vipo katika Mkoa wa Katavi, hususani vile vya Karema, Mwese na Mishamu, napenda kujua hayo.

Name

George Boniface Simbachawene

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibakwe

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS (TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA): Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza kabisa ameuliza ni lini hospitali hii ya Mkoa itakamilika kwa sababu hospitali ya Mpanda ambayo ni ya Wilaya sasa ndiyo inayotumika kwa ajili ya kutoa huduma hizo za Kimkoa. Je, ni hatua gani za dharura ambazo Serikali inaweza kuzichukua kwamba tutajaribu kuona na kwa kushirikiana na Halmashauri ya Wilaya ya Mpanda namna ambavyo tunaweza tukaiongezea uwezo wa dharura hiyo hospitali ya Wilaya ili kuweza kumudu majukumu ya Kimkoa. Hata hivyo, bado narudia kusema jibu la suluhu ya kudumu katika jambo hili ni kuhakikisha kwamba tunajenga hospitali hii na ndiyo maana Serikali inaendelea kutenga fedha kwaajili ya kujenga hospitali ya Mkoa huo.
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili ameuliza je, kama kuna vituo vya afya ambavyo vinaweza vikasaidia kupunguza uzito huu wa wagonjwa katika hospitali hii ya Wilaya ambayo sasa inatumika kama hospitali ya Mkoa. Ni kweli Serikali tumejipanga na tutajaribu kuona kwa vipaumbele na kwa maeneo
aliyoyasema kama tunaweza tukaanza na vituo hivyo kutokana na bajeti iliyotengwa kwa ajili ya Halmashauri ya Mpanda.

Name

Grace Sindato Kiwelu

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MOSHI S. KAKOSO aliuliza:- Hospitali ya Wilaya ya Mpanda ndiyo pekee inayotoa huduma za Mkoa katika Mkoa wa Katavi, kwa kutumia bajeti ya Halmashauri ya Wilaya ya Mpanda; Je, ni lini Hospitali ya Mkoa itajengwa?

Supplementary Question 2

MHE. GRACE S. KIWELU: Mheshimiwa Naibu Spika nakushukuru. Mheshimiwa Waziri hospitali yetu ya Wilaya ya Siha haina wodi ya watoto wala ya wazazi na hii inasababisha msongamano mkubwa sana katika hospitali yetu ya Mkoa ya Mawenzi.
Je, ni lini fedha hizo zitatoka ili ujenzi huo uanze mara moja?

Name

George Boniface Simbachawene

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibakwe

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS (TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA): Mheshimiwa Naibu Spika, sikumsikia amesema hospitali ipi?
MHE. GRACE S. KIWELU: Hospitali ya Wilaya ya Siha.
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS (TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA): Mheshimiwa Naibu Spika, sitaki nisiamini kwamba kweli hakuna wodi kwa ajili ya watoto na wazazi na kama kweli hakuna basi ni jambo ambalo linahitaji udharura wa hali yake.
Mheshimiwa Naibu Spika, mipango mingi ya vipaumbele katika sekta mbalimbali za huduma za jamii inapangwa kenye Halmashauri zetu. Kwa hivyo, tutajaribu kuona ni kwa namna gani wamepanga vipaumbele vyao na kwa sababu bajeti ya Wizara yangu imeshapitishwa na kwa maana ya Halmashauri zote nchini, basi tuweze kuona tunaweza tukaanza na hivi ambavyo ni muhimu zaidi katika sekta ya afya, kwa sababu kweli ni jambo gumu kidogo kuonekana kwamba hakuna wodi kwa ajili ya watoto na wazazi katika hospitali ambayo ina hadhi ya kuwa hospitali ya Wilaya. Kwa hiyo, nitalichukulia very seriously na kulishughulikia jambo hilo.

Name

Ally Mohamed Keissy

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nkasi Kaskazini

Primary Question

MHE. MOSHI S. KAKOSO aliuliza:- Hospitali ya Wilaya ya Mpanda ndiyo pekee inayotoa huduma za Mkoa katika Mkoa wa Katavi, kwa kutumia bajeti ya Halmashauri ya Wilaya ya Mpanda; Je, ni lini Hospitali ya Mkoa itajengwa?

Supplementary Question 3

MHE. ALLY K. MOHAMED: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana.
Kituo cha afya cha Kirando kilianzishwa miaka 42 iliyopita wakati Kirando ikiwa ni Kijiji, leo kina wakazi mara 50 zaidi kutoka miaka 42, aliyekuwa Waziri wa Afya Mheshimiwa Dkt. Seif Rashid alifika pale Kirando na akaniahidi kwamba hiki kituo kweli kimezidiwa na ninafanya mpango wa kuwa hospitali kamili.
Lini Serikali yako itaipa hadhi kituo cha afya Kirando kuwa hospitali kamili kwa kuwa kimezidiwa na wagonjwa?

Name

George Boniface Simbachawene

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibakwe

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS (TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA): Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli inawezekana kabisa kwamba katika huduma za vituo mbalimbali vya afya kumekuwa na kuzidiwa kwa sababu ya umbali kutokana na maeneo yetu kati ya kituo kimoja hadi kingine. Lakini kwa
suala la kituo cha afya ya Kirando ambacho Mheshimiwa Mbunge anasema kwamba kimezidiwa na je ni lini au kuna mikakati gani ya kuimarisha ili kiweze kutoa huduma hiyo au kubadilishwa kuwa hospitali.
Mheshimiwa Naibu Spika, nadhani kikubwa hapa ni ushirikiano kati ya mamlaka ya Serikali za Mitaa ambapo Waheshimwia Wabunge ni Madiwani kule katika kupanga vipaumbele vyetu, ni vizuri mkawa mnaturahisishia kazi ya kupanga halafu mnajua kabisa kwamba hatua zile huwa ikitoka pale mnaenda kwenye Mkoa ambapo mnashauriana, katika Sekretarieti ya Mkoa kwenye kikao cha ushauri cha Mkoa pale ndipo ambao mnaweza mkaja na mapendekezo halafu Serikali Kuu tukaona tuanze na lipi katika eneo lenu.
Mheshimiwa Ally Keissy, nikuombe tu kwamba kama mtasema tukiimarishe hiki na kuwa hospitali, basi jambo hili lije kwa utaratibu wa kisheria kama ulivyoelezwa katika Sera ya Afya.