Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 18 Sitting 1 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 2 2020-01-28

Name

Ruth Hiyob Mollel

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. RUTH H. MOLLEL aliuliza:-

Shule ya Msingi Vikindu katika Wilaya ya Mkuranga ina mikondo miwili (A na B) darasa la kwanza hadi la saba na mwaka 2019 darasa la kwanza na la pili yalikuwa na wanafunzi 300 kila darasa.

(a) Je, Serikali ina mkakati gani kuhakikisha uwiano wa mwalimu na mwanafunzi wa 1:45 unazingatiwa kwa mujibu wa Sera ya Elimu ya Msingi?

(b) Je, kwa msongamano huo tunaweza kupata wanafunzi walioelimika na kukidhi malengo ya Tanzania ya viwanda?

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. MWITA M. WAITARA) alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Ruth Hiyob Mollel, Mbunge wa Viti maalum kama ifuatavyo swali lake ambalo lina sehemu (a) na (b):-

(a) Mheshimiwa Spika, ongezeko la uandikishaji wa wanafunzi katika Halmashauri ya Mkuranga limetokana na juhudi za Serikali za kuhamasisha wananchi kuandikisha wanafunzi shuleni kupitia mpango wa elimu msingi bila malipo. Ili kukabiliana na msongamano wa wanafunzi katika Shule za Msingi Vikindu, Serikali imechukua hatua mbalimbali ikiwemo kujenga Kituo Shikizi cha Juhudi, Kitwangi, Mitawa na Muungano. Kituo Shikizi cha Muungano kilichopo katika Kijiji cha Vikindu kinatarajiwa kukamilika mwezi Februari, 2020 na kitakuwa na uwezo wa kupokea wanafunzi 300. Mkakati mwingine ni wanafunzi kusoma kwa kupokezana yaani double section ambapo kuna madarasa ya asubuhi na ya mchana.

(b) Mheshimiwa Spika, kama ilivyoelezwa kwenye sehemu (a) hatua mbalimbali zimechukuliwa na zinaendelea kuchukuliwa na Serikali ili kuhakikisha msongamano wa wanafunzi madarasani unapungua na kuwezesha kupata elimu bora. Ahsante.