Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Ruth Hiyob Mollel

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. RUTH H. MOLLEL aliuliza:- Shule ya Msingi Vikindu katika Wilaya ya Mkuranga ina mikondo miwili (A na B) darasa la kwanza hadi la saba na mwaka 2019 darasa la kwanza na la pili yalikuwa na wanafunzi 300 kila darasa. (a) Je, Serikali ina mkakati gani kuhakikisha uwiano wa mwalimu na mwanafunzi wa 1:45 unazingatiwa kwa mujibu wa Sera ya Elimu ya Msingi? (b) Je, kwa msongamano huo tunaweza kupata wanafunzi walioelimika na kukidhi malengo ya Tanzania ya viwanda?

Supplementary Question 1

MHE. RUTH H. MOLLEL: Mheshimiwa Spika, naomba kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, Shule Shikizi ya Muungano ilijengwa na nguvu za wananchi kwa muda mrefu na mpaka leo tunaambiwa kwamba hiyo shule itakamilika Februari. Je, Serikali haina takwimu za wanafunzi wanaomaliza kusudi hii miundombinu ianze kutengenezwa mapema ili wanafunzi waweze kwenda kwenye shule zao?

Mheshimiwa Spika, swali langu la pili; je, umeme ni lini utaunganishwa katika hiyo shule? Ahsante.

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. MWITA M. WAITARA): Mheshimiwa Spika, swali la kwanza angependa kujua kama Serikali ina takwimu; naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba Serikali ina takwimu za idadi ya wanafunzi ambao wapo katika maeneo yetu mablimbali nchini.

Mheshimiwa Spika, vilevile katika eneo hili, Jimbo la Mkuranga kwa Mheshimiwa Abdallah Ulega pamoja na Mheshimiwa Mbunge na wengine wamefanyakazi kubwa sana ya kusaidia na kuchangia kupitia Mfuko wa Jimbo, wadau mbalimbali na Mbunge mwenzake wa Viti Maalum katika Mkoa ule wamefanyakazi kubwa sana ya ziada. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, lakini naomba nimwmabie Mheshimiwa Mbunge kwamba tumeshafanya tathmini, tunajua ni kweli kwa mwaka huu wanafunzi baadhi walibaki kwa muda mrefu nyumbani baada ya kuwa na upungufu wa miundombinu, lakini tulivyofanya tathmini sasa hivi tumekubaliana, tumefanya projection kwamba hii changamoto ya miundommbinu itakwenda kupungua, lakini tushirikiane, Serikali, Wabunge, wadau mbalimbali ili tuweze kuboresha miundombinu yetu hii. Ni matarajio yetu ni kwamba hii hali ya kuwa na uoungufu itaendelea kupungua kadri muda utakavyokuwa unakwenda.

Mheshimiwa Spika, lakini jambo la pili, ametaka kujua kama ni lini umeme utaunganishwa katika shule hii; naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba suala la umeme ni suala ambalo sisi wote tushirikishane pale kwa sababu hii ni sehemu ya umma tunatoa huduma. Lakini kwamba tutaweza kuweka miundombinu katika shule zote haiwezekani kwa maana ya Serikali sisi wenyewe. Mheshimiwa Mbunge ni mdau muhimu na wadau wengine wote tushirikiane tuone, tujue ni kiasi gani kinaweza kikasaidia shule hii kupata umeme ili tuweke katika eneo hilo. Ahsante.

Name

Susan Anselm Jerome Lyimo

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. RUTH H. MOLLEL aliuliza:- Shule ya Msingi Vikindu katika Wilaya ya Mkuranga ina mikondo miwili (A na B) darasa la kwanza hadi la saba na mwaka 2019 darasa la kwanza na la pili yalikuwa na wanafunzi 300 kila darasa. (a) Je, Serikali ina mkakati gani kuhakikisha uwiano wa mwalimu na mwanafunzi wa 1:45 unazingatiwa kwa mujibu wa Sera ya Elimu ya Msingi? (b) Je, kwa msongamano huo tunaweza kupata wanafunzi walioelimika na kukidhi malengo ya Tanzania ya viwanda?

Supplementary Question 2

MHE. SUSAN A. J. LYIMO: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa nafasi.

Mheshimiwa Spika, suala hili la upungufu wa madarasa limekuwa likijirudia mara kwa mara na Waziri anasema wana takwimu. Mwaka juzi wanafunzi 133,000 walifaulu lakini wakashindwa kuchanguliwa kwa sababu ya madarasa, lakini mwaka huu tena zaidi ya wanafunzi 58,000 wamefaulu darasa la saba lakini wamekosa madarasa.

Mheshimiwa Spika, swali langu, ni kwa sababu gani Serikali kama ina projection na inajua ni wanafunzi wangapi wanaweza kufaulu na wako darasa la saba, ni kwa sababu gani hawana mpango mahususi kuhakikisha kwamba kila mwaka wanatenga fedha kwa ajili ya madarasa ili angalau kwa miaka mitano tuhakikishe kwamba tatizo hili sugu limekwisha na wanafunzi wetu wanapomaliza darasa la saba wanakwenda shuleni kama wengine. Kwa sababu tunavyozungumza leo kuna Wanafunzi Dar es Salaam na Mikoa mingine wamefaulu darasa la saba lakini watakwenda kuanza mwezi wa tano, haoni kwamba hili ni tatizo? Ahsante sana.

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Spika, kwanza naomba nimshukuru dada yangu Mheshimiwa Susan Lyimo kwa sababu amekuwa na mchango mkubwa sana katika elimu.

Mheshimiwa Spika, Serikali inafanya kila liwezekanalo na kwa mfano, mwaka huu tulikuwa na wanafunzi takribani 759,000 waliofaulu na hii inaonekana kutokana na juhudi kubwa ndiyo maana mwaka huu ufaulu umepanda kwa wastani wa asilimia 3.7 ambayo ni mafanikio makubwa sana yaliyowahi kutokea.

Mheshimiwa Spika, ndiyo maana licha ya ufaulu huo ulikuwa mkubwa lakini zaidi ya asilimia 92 na wanafunzi wote tuliowachangua katika awamu ya kwanza tulibakisha wanafunzi 58,000 ambao hata hivyo wanafunzi wote hivi sasa tumeshawachangua na hivi sasa kuna shughuli kubwa sana ya umaliziaji baadhi ya madarasa 1,080 ambayo naomba niwahakikishie Watanzania kwamba ukiona juhudi wanafunzi wanafaulu ni impact kubwa ya Serikali ya uwekezaji iliyosababisha mpaka wanafunzi waweze kufaulu zaidi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, tushikamane kwa pamoja kuona ufaulu mkubwa kwetu sisi iwe ni mafanikio makubwa kwamba Tanzania inasonga mbele katika suala zima la kuhakikisha kila Mtanzania anapata elimu. Ahsante.