Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 18 Sitting 5 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 53 2020-02-03

Name

Edwin Mgante Sannda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kondoa Mjini

Primary Question

MHE. EDWIN M. SANNDA aliuliza:-

Maboma mengi ya maabara kwenye Shule za Sekondari za Kata nchini hayajakamilika na hata pale yanapokamilika hakuna vifaa vya maabara na tunahitaji sana wanasayansi kuelekea uchumi wa viwanda:-

(a) Je, Serikali ina mkakati gani wa kukamilisha maabara hizo na lini zitakamilika?

(b) Je, ni lini vifaa vitapelekwa katika maabara zilizokamilika?

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NCHI, OFlSI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. MWITA M. WAITARA) alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais-TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Edwin Mgante Sannda, Mbunge wa Kondoa Mjini, lenye sehemu (a) na (b) kama ifuatavyo:-

(a) Mheshimiwa Spika, Serikali kwa kushirikisha nguvu za wananchi na Washirika wa Maendeleo imekamilisha ujenzi wa maabara 5,801 kati ya maabara 11,369 zinazohitajika. Hivyo, upungufu uliopo ni maabara 5,568. Serikali inaendelea na ukamilishaji wa vyumba vya maabara kupitia ruzuku ya Serikali Kuu na mapato ya ndani kwa kushirikisha nguvu za wananchi. Vilevile, katika mwaka wa fedha 2019/2020, Halmashauri ya Kondoa Mji, imeidhinishiwa jumla ya Sh. 8,000,000 kwa ajili ya ukamilishaji wa maabara katika Shule ya Sekondari Bicha.

(b) Mheshimwa Spika, Serikali imenunua na kusambaza vifaa vya maabara vyenye thamani ya shilingi bilioni 19.13 katika shule 2,948 za sekondari zilizokamilisha ujenzi wa maabara. Serikali kwa kushirikisha wananchi na wadau wa maendeleo itaendelea kuboresha maabara za masomo ya sayansi ili ufundishaji wa masomo hayo ufanyike kwa vitendo na siyo nadharia.