Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 18 Sitting 6 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 67 2020-02-04

Name

Pascal Yohana Haonga

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Mbozi

Primary Question

MHE. PASCAL Y. HAONGA aliuliza:-

Wastani wa akinamama wanaojifungua kwa siku ni 18 - 20 katika Hospitali ya Wilaya ya Mbozi; licha ya idadi kubwa ya akinamama wanaojifungua, kuna ufinyu wa majengo mbalimbali ikiwepo na wodi ya akinamama:-

(a) Je, ni lini Serikali itashughulikia ujenzi wa wodi ya akina mama katika hospitali hii?

(b) Hospitali ya Wilaya ya Mbozi inatumika kama Hospitali ya Mkoa wa Songwe na haina maji safi na salama. Je, ni lini Serikali itapeleka huduma ya maji safi na salama katika hospitali hii?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE) alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Pascal Yohana Haonga, Mbunge wa Mbozi lenye sehemu (a) na (b) kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, Halmashauri ya Wilaya ya Mbozi imefanya tathmini na kubaini zinahitajika jumla ya shilingi milioni 37 kwa ajili ya upanuzi wa wodi ya akina mama wanaojifungua. Mradi huo umepewa kipambele katika mpango wa bajeti wa mwaka 2020/2021 ili kuanza ujenzi.

Katika mwaka wa fedha 2019/2020 Halmashauri imeidhinishiwa jumla ya shilingi milioni 12 kwa ajili ya kuchimba kisima cha maji katika hospitali ya Wilaya ya Mbozi ili kutatua changamoto ya maji katika hospitali hiyo.