Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Pascal Yohana Haonga

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Mbozi

Primary Question

MHE. PASCAL Y. HAONGA aliuliza:- Wastani wa akinamama wanaojifungua kwa siku ni 18 - 20 katika Hospitali ya Wilaya ya Mbozi; licha ya idadi kubwa ya akinamama wanaojifungua, kuna ufinyu wa majengo mbalimbali ikiwepo na wodi ya akinamama:- (a) Je, ni lini Serikali itashughulikia ujenzi wa wodi ya akina mama katika hospitali hii? (b) Hospitali ya Wilaya ya Mbozi inatumika kama Hospitali ya Mkoa wa Songwe na haina maji safi na salama. Je, ni lini Serikali itapeleka huduma ya maji safi na salama katika hospitali hii?

Supplementary Question 1

MHE. PASCAL Y. HAO NG A: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la kwanza; kwa kuwa katika majibu ya Serikali ni kwamba zimetengwa milioni 37 zitakazotumika katika kuboresha wodi ya akina mama wanaojifungua; na kwa kuwa wodi hiyo ni wodi ambayo kwa kweli akina mama wanapata shida, wanalala akina mama wawili katika kitanda kimoja na kuna msongamano mkubwa sana;

Je, Serikali sasa inaweza ikatupa majibu rasmi wana Mbozi na wana Songwe kwamba hizo fedha ni lini sasa zitakwenda rasmi? Kwasababu tatizo hili si dogo, ni kubwa sana. Akina mama wanapata shida na wanaweza kupata magonjwa kwasababu kuna msongamano ambao kwa kweli si wa kawaida?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili; kwa kuwa pia katika Hospitali hii ya Wilaya ya Mbozi ambayo pia inatumika kama Hospitali Teule ya Mkoa wa Songwe kuna tatizo la ufinyu wa OPD; na OPD iliyopo pale ni ndogo sana na kuna msomngamano mkubwa sana.

Je, Serikali ipo tayari sasa kufanya upanuzi wa ile OPD ili iweze kuboreshwa na ichukue wagonjwa walio wengi zaidi kuliko hali iliyoko sasa ambayo wagonjwa ni wengi na OPD ni ndogo?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nichukue fursa hii kujibu maswali yote mawili ya Mheshimiwa Haonga kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika majibu yangu ya msingi nimemwmbia Mheshimiwa Mbunge commitment ya Serikali kwamba katika bajeti ya mwaka 2020/2021 milioni 37 zimetengwa. Tafsiri yake ni nini? Ni kwamba hiyo inaonesha seriousness ya Serikali katika kuahidi na kuweka katika maandishi. Naomba Mheshimiwa Mbunge aendelee kuiamini Serikali, tukiahdi tunatekeleza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika swali lake la pili anaongelea juu ya suala zima la ufinyu wa wodi, kwa maana kunakuwa na msongamano mkubwa wa wagonjwa katika ile hospitali ambayo inatumika kama ndiyo hospitali ya rufaa ya Mkoa. Ni ukweli usiopingika kwamba hospitali ile mwanzo haikuwa imekusudiwa kuwa hospitali ya Mkoa; lakini pia ni ukweli usiopingika Serikali imekuwa ikifanyakazi kubwa sana ya kuhakikisha kwamba huduma ya afya inasogezwa na ndiyo maana hata ukienda kwa Mheshimiwa Haonga unakuta kuna kituo cha afya cha Kisansa ambacho tukienda tukafanya shughuli nzuri na yeye ni shuhuda. Aendelee kuiamini Serikali, kwamba tutafanya kila liwezekanalo kuhakikisha kwamba pale ambapo inahitajika tufanye upanuzi tutafanya pasi na kusita.

Name

George Malima Lubeleje

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpwapwa

Primary Question

MHE. PASCAL Y. HAONGA aliuliza:- Wastani wa akinamama wanaojifungua kwa siku ni 18 - 20 katika Hospitali ya Wilaya ya Mbozi; licha ya idadi kubwa ya akinamama wanaojifungua, kuna ufinyu wa majengo mbalimbali ikiwepo na wodi ya akinamama:- (a) Je, ni lini Serikali itashughulikia ujenzi wa wodi ya akina mama katika hospitali hii? (b) Hospitali ya Wilaya ya Mbozi inatumika kama Hospitali ya Mkoa wa Songwe na haina maji safi na salama. Je, ni lini Serikali itapeleka huduma ya maji safi na salama katika hospitali hii?

Supplementary Question 2

MHE. GEORGE M. LUBELEJE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi ili na mimi niweze kuuliza swali moja la nyongeza:-

Kwa kuwa hospitali ya Wilaya Mpwapwa ilijengwa Mwaka 1975 na kwa kuwa wodi ya Wakina Mama wanaojifungua ni ndogo. Kama walivyosema wenzangu akina mama wanalala wawili, wanalala watatu ambapo ni hatari kaisa kuambukizana magonjwa.

Je, Mheshimiwa Waziri katika bajeti inayokuja, utatenga fedha kwa ajili ya kujenga jengo kubwa la wodi ya akina mama katika Hospitali ya Wilaya ya Mpwapwa?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nijibu swali la Mheshimiwa Seneta Lubeleje kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni ukweli usiopingika kwamba hospitali za wilaya zilizojengwa miaka ya zamani ukilinganisha na uhalisia wa sasa hivi kumekuwa na upungufu wa baadhi ya majengo au msongamano umekuwepo kwasababu idadi ya watu inaongezeka. Naomba Mheshimiwa Mbunge akubaliane na kazi nzuri ambayo inafanya na Serikali. Tumeanza na hizo hospitali 67; kwa kadri Bajeti itakavyoruhusu na uhalisia na kwake pia tutatazama nini cha kufanya.

Name

Joseph Roman Selasini

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Rombo

Primary Question

MHE. PASCAL Y. HAONGA aliuliza:- Wastani wa akinamama wanaojifungua kwa siku ni 18 - 20 katika Hospitali ya Wilaya ya Mbozi; licha ya idadi kubwa ya akinamama wanaojifungua, kuna ufinyu wa majengo mbalimbali ikiwepo na wodi ya akinamama:- (a) Je, ni lini Serikali itashughulikia ujenzi wa wodi ya akina mama katika hospitali hii? (b) Hospitali ya Wilaya ya Mbozi inatumika kama Hospitali ya Mkoa wa Songwe na haina maji safi na salama. Je, ni lini Serikali itapeleka huduma ya maji safi na salama katika hospitali hii?

Supplementary Question 3

MHE. JOSEPH R. SELASINI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na jitihada za Serikali katika kujenga vituo vya afya na hospitali lakini vilevile vifaatiba pamoja na wataalam ni muhimu sana; na muhimu zaidi ni elimu kwa Watanzania namna ya kutumia hizi hospitali na vituo vya afya. Kwasababu tumeshuhudia sasa hivi wamezuka watu wanawadanyanya Wananchi wavue nguo zao za ndani wapungie juu wapate ujauzito, sijui wanawanyweshwa jiki na vitu kama hivyo vya aibu tena wanaofanyiwa aibu hizi ni akina mama.

Je, Serikali ina mkakati gani wa kutoa elimu kwa Watanzania ili wajue wkamba kuna mambo ambayo yanahitaji utaalam wa kidaktari na si uongo wa watu wanaojiita manabii na wachungaji wanaodhalilisha Watanzania katika mambo mbalimbali?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nijibu swali la Mheshimiwa Joseph Raman Selasini, Mbunge wa Rombo kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la kujenga vituo vya afya na kupeleka huduma ya afya kama haitumiki hata umaana wenyewe unakua haupo. Naomba nikubaliane an Mheshimiwa Mbunge Selasini; lakini pia tukubaliane kwamba hii kazi si kazi ya Serikali peke yake. Sisi Waheshimiwa Wabunge tuna fursa katika forum mbalimbali ambazo tunakutana nazo, ni vizuri tukatoa elimu lakini pia hata maeneo ya makanisa, misikiti ni vizuri elimu ikapelekwa; si suala la kuiachia Serikali peke yake lakini pia Serikali haikwepi wajibu wa kuhakikisha wkamba elimu inapelekwa kwa wananchi.

Name

Joseph Kasheku Musukuma

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Geita

Primary Question

MHE. PASCAL Y. HAONGA aliuliza:- Wastani wa akinamama wanaojifungua kwa siku ni 18 - 20 katika Hospitali ya Wilaya ya Mbozi; licha ya idadi kubwa ya akinamama wanaojifungua, kuna ufinyu wa majengo mbalimbali ikiwepo na wodi ya akinamama:- (a) Je, ni lini Serikali itashughulikia ujenzi wa wodi ya akina mama katika hospitali hii? (b) Hospitali ya Wilaya ya Mbozi inatumika kama Hospitali ya Mkoa wa Songwe na haina maji safi na salama. Je, ni lini Serikali itapeleka huduma ya maji safi na salama katika hospitali hii?

Supplementary Question 4

MHE. JOSEPH K. MUSUKUMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakuskhuru sana kwa kunipa nafasi na mimi niweze kuulizwa swali la nyongeza.

Jimbo la geita Vijijini lina population ya watu takribani 450,000 mpaka 500,000 na halina Kituo cha afya hata kimoja. Je, Serikali haioni umhimu wa kutupatia kituo chaafya katika Kijiji cha Ibisabageni, Tarafa ya Isuramtundwe kwa ajili ya kuokoa wale akina mama wanaosafiri kwa umbali wa Kilometa 80 kuipata hospitali ya Wilaya?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nijibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Musukuma kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza naomba uniruhusu kwa dhati kabisa nimpongeze Mheshimiwa Musukuma jinsi ambavyo amekuwa akipigania suala zima lafya na yeye amekuwa akijinasibu kwamba katika maeneo ambayo yamefanikiwa kujengwa hospitali nzuri ya Wilaya ni pamoja na kwenye Jimbo lake.

Mheshimiwa Mwenyekiti, adhma ya Serikali ni kuhakikisha kwamba inasogeza huduma za afya kwa wananchi. Naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge, kama ambavyo amekuwa akitoa imani kwa Serikali azidi kuiamini kwamba pale ambapo wananchi na hasa sehemu ambayo population ni kubwa kama ambavyo ametaja katika eneo lake hakika kwa kadri bajeti itakavyokuwa inaruhusu kwa siku za usoni na wao tutawajengea kituo cha afya.