Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 18 Sitting 6 Water and Irrigation Wizara ya Maji 76 2020-02-04

Name

Bupe Nelson Mwakang'ata

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. BUPE N. MWAKANG‟ATA aliuliza:-

Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga visima virefu vya maji katika Wilaya ya Nkasi ili kutatua changamoto ya maji iliyopo?

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Maji naomba kujibu swali la Mheshimiwa Bupe Nelson Mwakang‟ata Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kutambua tatizo la maji lililopo katika Wilaya ya Nkasi Serikali katika mwaka wa fedha 2019/2020 imepanga kuchimba visima virefu 9 katika maeneo ya Masolo, Katogolo, Mpata, Mienge, Itindi, Kacheche, Lyele, Mbwendi na Kakoma. Kiasi cha shilingi milioni 315 kimetengwa katika bajeti ya mwaka 2019/2020 kwa ajili ya kazi hiyo. Hadi kufikia mwezi Disemba 2019, Visima 7 vimechimbwa katika vijiji vya Masolo, Katogolo, Mpata, Mienge, Kanazi na Ipanda na kiasi cha shilingi milioni 220 kimetumika katika upimaji na uchimbaji wa visima hivyo ambavyo vitatumika kama vyanzo vya maji katika vijiji husika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika mpango wa muda mrefu wa kutatua tatizo la maji katika Wilaya ya Nkasi, katika mwaka wa fedha 2019/2020, Serikali imepanga kutumia zaidi ya bilioni 1.3 kwa kupitia Programu ya PforR kwa ajili ya kuboresha huduma ya maji katika Wilaya ya Nkasi. Wizara imeshatuma fedha hizo kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya maji 6 Wilayani Nkasi ambapo miradi yote hiyo itatekelezwa kwa mfumo wa wataalam wa ndani (Force Account).