Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Bupe Nelson Mwakang'ata

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. BUPE N. MWAKANG‟ATA aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga visima virefu vya maji katika Wilaya ya Nkasi ili kutatua changamoto ya maji iliyopo?

Supplementary Question 1

MHE. BUPE N. MWAKANG‟ATA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante nashukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza kabisa naomba nichukue nafasi hii kuipongeza sana Serikali ya Awamu ya Tano chini ya Kiongozi Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli. Kwa kazi kubwa ya kuweza kumtua mama ndoo kichwani. Serikali hii imewaza kutuliza hata ndoa za wanawake wa Tanzania, wameweza kutulia kwa sababu maji yanapatikana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya pongezi hizi sasa naomba niulize maswali mawili ya nyongeza;

(i) Wilaya ya Nkasi ina takribani ya vijiji 35 wanaoishi pembezoni mwa Ziwa Tanganyika, na wanatumia maji ya ziwa Tanganyika ambayo yanawasababishia kupata magonjwa mbalimbali ikiwemo kipindupindu na magonjwa ya kuhara. Sasa ni lini sasa Serikali itawajengea visima virefu ambavyo vitawasababisha wapate maji salama?

(ii) Wilaya ya Nkasi imegawanyika katika sehemu mbili, Nkasi Kusini na Nkasi Kaskazini. Naishuruku Serikali imeweza kujenga visima 9 ambavyo sasa hivi vinaendelea kujengwa, lakini bado Nkasi Kusini ambavyo havijajengwa visima takribani 7 ambavyo tuliomba kijiji cha Masolo, Kijiji cha Milindikwa, Malongwe, Sintali, Nkana na vijiji vingine bado havijachimbiwa visima.

Je, nili sasa Serikali itachimba visima hivyo?

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nimpongeze Mheshimiwa Mbunge amekuwa mpiganaji mkubwa hususani kwa kina mama wa Mkoa wake wa Rukwa. Lakini nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge sisi kama Wizara ya Maji hatuta kuwa kikwazo kwa Mkoa wa Rukwa na Nkasi katika kuhakisisha wanapata maji. Ziara ya Mheshimiwa Waziri katika Jimbo la Nkasi kwa Mheshimiwa Kessy alilia sana pale Mheshimiwa Mbunge na tumetoa fedha kwa ajili ya utekelezaji wa miradi mikubwa katika mji wa Kilando pamoja na Namanyele zaidi ya milioni tano kwa ajili ya miradi ile mikubwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia tumepata fedha za PforF zaidi ya bilioni nne kwa Mkoa wa Rukwa, tumepeleka bilioni 1.3 katika Wilaya ya Nkasi katika kuhakikisha tunakwenda kutatua tatizo la maji. Naomba Waheshimiwa Wabunge waende kusimamia miradi ile katika kuhakikisha wakinamama wanaendelea kutua na ndoo kichwani na ndoa zao zinaendelea kuimarika. Ahsante sana.