Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 18 Sitting 7 Energy and Minerals Wizara ya Madini 92 2020-02-05

Name

Aida Joseph Khenani

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Nkasi Kaskazini

Primary Question

MHE. AIDA J. KHENANI aliuliza:-

Je, kwa sasa Tanzania ina aina ngapi za madini?

Name

Doto Mashaka Biteko

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukombe

Answer

WAZIRI WA MADINI alijibu:-

Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Aida Joseph Khenani, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Tanzania ina aina mbalimbali za madini ambayo kijiosayansi yamegawanyika katika makundi matano ambayo ni; madini ya metali kama vile dhahabu, madini ya fedha, chuma, shaba, risasi, aluminum, nickel, niobium, bati na kadhalika.

Mheshimiwa Spika, yako pia aina nyingine ya madini, ambayo ni madini ya vito (gemstones) ambayo ni pamoja na madini ya Tanzanite, almasi, rubi pamoja na mengineyo

Mheshimiwa Spika, kundi la tatu ni la madini ya viwandani, ambayo yanaintwa industrial minerals kama vile kaolin, mawe ya chokaa, jasi, phosphate pamoja na chumvi na na mchanga wa ufukweni.

Mheshimiwa Spika, madini ya ujenzi ni kundi lingine la madini ambayo ni madini ya nakshi kama vile mawe, kokoto, udongo wa mfinyanzi, mchanga na mawe ya nakshi. Aidha, yapo pia madini ya nishati kama vile makaa ya mawe, gesi na uranium.

Mheshimiwa Spika, madini haya ni muhimu katika kujenga uchumi wa viwanda na kuongeza mchango wa uchumi kwa madini katika Pato la Taifa. Madini haya ni muhimu katika maendeleo ya wananchi kwa kuwa yanatumika katika shughuli mbalimbali za ujenzi, viwanda, mapambo na kuleta fedha za kigeni nchini.