Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 18 Sitting 9 Water and Irrigation Wizara ya Maji 116 2020-02-07

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Primary Question

MHE. DAVID E. SILINDE aliuliza:-

Je, Serikali ina mpango gani kwa sasa kutatua kero ya maji kwa uhakikia katika Jimbo la Momba?

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Maji, naomba kujibu swali la Mheshimiwa David Ernest Silinde, Mbunge wa Momba, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, katika juhudi za kutatua tatizo la maji katika Jimbo la Momba, Serikali inaendelea kutekekeza miradi mitatu katika Vijiji vya Ndalambo ambapo ujenzi umekamilika kwa asilimia 95, Kijiji cha Chitete ujenzi umekamilika kwa asilimia 12 na Tindingomba ujenzi umekamilika kwa asilimia 80. Miradi hii ikikamilika, itahudumia jumla ya watu wapatao 23,397 na kuongeza upatikanaji wa huduma ya maji safi, salama kwa wananchi.

Mheshimiwa Naibu Spika, aidha, Serikali imeanza kutekeleza miradi ya vijiji vitano kupitia Programu ya Malipo kwa Matokeo (PfR) katika Vijiji vya Mkulwe, Chiwanda, Kasinde, Ikana na Namsinde II kwa gharama ya Sh.805,885,340. Kukamilika kwa miradi hii, kutawezesha jumla ya watu 31,984 kupata huduma ya maji.