Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 16 Sitting 5 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 57 2019-09-09

Name

Fakharia Shomar Khamis

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. FAKHARIA SHOMAR KHAMIS aliuliza:-

Askari wa Jeshi la Polisi Zanzibar (Ziwani) wanakabiliwa na matatizo makubwa ya makazi kama vile miundombinu ya maji, nyumba chakavu, uhaba wa vyoo na kuharibika kwa uzio uliokuwepo katika eneo hilo unaohatarisha usalama wao:-

(a) Je, kuna mpango gani wa kufanyia matengenezo nyumba na vyoo kwa wakati huu?

(b) Je, Uzio wa boma hilo la Ziwani utafanyiwa ukarabati?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Fakharia Shomar Khamis, Mbunge wa Viti Maalum lenye sehemu (a) na (b) kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Jeshi la Polisi linakabiliwa na tatizo la uchakavu wa miundombinu kama majengo ya ofisi na nyumba za kuishi Askari kutokana na kuwa ya muda mrefu. Serikali kupitia Jeshi la Polisi imekuwa ikifanya ukarabati wa miundombinu hiyo kwa awamu ili kuboresha huduma kwa wananchi Mheshimiwa Spika Mipango ya ukarabati ya miundombinu hiyo kwa awamu ili kuboresha huduma kwa wananchi.

Mheshimiwa Spika, mipango ya ukarabati wa miundombinu katika Kambi hiyo imeanza kwa kuandaa makadirio ya ukarabati kwa kuzingatia vipaumbele hasa kwa nyumba ambazo zimechakaa na ambazo zinaweza kukarabatika, mahitaji na gharama za majengo husika.

Mheshimiwa Spika, uzio wa Kambi ya Polisi - Ziwani ni wa fensi ya waya ambayo imezunguka eneo kubwa na waya huu katika baadhi ya maeneo ambao umechoka na kuchakaa kabisa. Aidha, upo mpango wa kujenga fensi ya matofali mara tu pale fedha zitakapokuwa zimepatikana.