Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 16 Sitting 6 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 71 2019-09-10

Name

Susan Limbweni Kiwanga

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Mlimba

Primary Question

MHE. SUSAN L. KIWANGA Aliuliza:-

Jimbo la Mlimba lina mito mingi mikubwa inayotenganisha kata pamoja na vijiji.

Je, ni lini TARURA itajenga madaraja ya kudumu katika Kata ya Mbingu na Kijiji cha Chiwachiwa, Kata ya Igima na Kijiji cha Mpofu, Kijiji cha Ngajengwa (kwa Mtwanga), Kata ya Mchombe na Kijiji cha Igia, Kata ya Mofu na Kijiji cha Ikwambi, Kata ya Mbingu, Kata ya Utengule na Kijiji cha Ipugasa, Kata ya Kamwene na Kata ya Uchindile, Kata ya Msagati Kijiji cha Taweta na Kijiji cha Tanga, Kata ya Kalengakelu na Merela, Kata ya Mlimba - Sokoni na Kata ya Idete – Barabara ya Itikinyu?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE) alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais – TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Susan Limbweni Kiwanga, Mbunge wa Mlimba kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali kupitia Wakala wa Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA) imeanza kushughulikia ujenzi wa vivuko katika Halmashauri ya Kilombero hususani Jimbo la Mlimba. Katika mwaka wa fedha 2018/2019 Serikali ilinunua na kuweka daraja la chuma katika Mto Kihansi linalounganisha Vijiji vya Chita, Idunda na Melera kwa gharama ya shilingi milioni 717.62. Kazi hiyo tayari imekamilika ikiwa ni hatua ya awali ya kuunganisha Kata za Chita na Kalengakele.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika bajeti ya mwaka 2019/2020 TARURA imetenga kiasi cha shilingi milioni 127.94 kwa ajili ya ujenzi wa madaraja/makalvati katika barabara za Miembeni - Vigaeni, Kichangani katika Kata za Mbingu, Namwawala - Mofu katika Kata ya Mofu, Iduindembo - Utengule katika Kata ya Utengule, Manyasini katika Kata ya Mlimba, Ngwasi - Uga katika Kata ya Kalengakelu na Uchindile.

Aidha, TARURA kwa kushirikiana na Mfuko wa Barabara (Road Fund) imeweza kutenga kiasi cha shilingi milioni 300 kwa ajili ya ujenzi wa daraja la mita 25 katika barabara ya Kisegese - Chiwachiwa - Lavena ambapo kwa sasa lipo katika hatua za upembuzi yakinifu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali itaendelea kutenga fedha na kujenga barabara, madaraja na makalvati kwa awamu kwa kadri ya upatikanaji wa fedha.