Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Susan Limbweni Kiwanga

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Mlimba

Primary Question

MHE. SUSAN L. KIWANGA Aliuliza:- Jimbo la Mlimba lina mito mingi mikubwa inayotenganisha kata pamoja na vijiji. Je, ni lini TARURA itajenga madaraja ya kudumu katika Kata ya Mbingu na Kijiji cha Chiwachiwa, Kata ya Igima na Kijiji cha Mpofu, Kijiji cha Ngajengwa (kwa Mtwanga), Kata ya Mchombe na Kijiji cha Igia, Kata ya Mofu na Kijiji cha Ikwambi, Kata ya Mbingu, Kata ya Utengule na Kijiji cha Ipugasa, Kata ya Kamwene na Kata ya Uchindile, Kata ya Msagati Kijiji cha Taweta na Kijiji cha Tanga, Kata ya Kalengakelu na Merela, Kata ya Mlimba - Sokoni na Kata ya Idete – Barabara ya Itikinyu?

Supplementary Question 1

MHE. SUSAN L. KIWANGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa majibu haya ingawa wamekosea sana majina ya vijiji vyangu na kata zangu na pale napenda kutoa marekebisho kwamba pale Taweta ni Kijiji cha Tanganyika siyo Tanga, sisi kwetu hatuna Tanga.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na jitihada za Serikali lakini jimbo la Mrimba lina changamoto kubwa sana ukizingatia sisi ni wakulima kama asilimia 99 kwa hiyo madaraja haya yasipojengwa kwa wakati kwa hiyo mazao mengi yanashindwa kufika sokoni na wakulima kuwa maskini miaka yote.

Je, pamoja na bajeti hii imetengwa, Serikali haioni kwamba iliangalie Jimbo la Mlimba kwa akina ya pekee kuhakikisha kwamba wananchi hawa wanapata miundombinu hii ukizingatia mito mingi mikubwa kwa mfano hii Tanganyika kuna huo Mto Kilombero ndiyo unapita huko, chini kuna mamba wengi lini mtafanya na kunatakiwa daraja kubwa.

Je, Waziri mara nyingi naongea na wewe upo tayari sasa kutembelea hilo Jimbo la Mlimba hivi uone hali halisi na uone kwamba kunajitihada za kujenga haya madaraja uone wananchi wanavyoteseka na mara nyingi nakuomba lakini hutaki kwenda? (Makofi)

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kwanza atuwie radhi kwa kukosea majina ya vijiji vyake hatukukusudia hilo, lakini na yeye mwenyewe amekiri kwamba tumetenga kiasi cha shilingi milioni 300 kwa ajili ya kuanza kujenga hilo daraja ambalo ni kubwa lakini kiasi cha shilingi 127; naomba Mheshimiwa Mbunge aridhike na jitihada ambazo zinafanywa na Serikali kwamba ni azma yetu kuhakikisha kwamba wananchi wa Mlimba wanapata madaraja na barabara za uhakika katika kipindi chote na mimi nashukuru, leo ameongea hajalia na sisi tunamhakikishia haitatokea kulia tena.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini Mheshimiwa Susan amesema amekuwa akiniomba twende Mlimba naomba nimhakikishie nipo tayara ilikuwa ni swala tu la muda tupange na yeye mwenyewe tumewasiliana kunapindi fulani akasema kipindi hiki mvua zinanyesha sana hatuwezi kwenda, niko tayari.

Name

Issaay Zacharia Paulo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Mjini

Primary Question

MHE. SUSAN L. KIWANGA Aliuliza:- Jimbo la Mlimba lina mito mingi mikubwa inayotenganisha kata pamoja na vijiji. Je, ni lini TARURA itajenga madaraja ya kudumu katika Kata ya Mbingu na Kijiji cha Chiwachiwa, Kata ya Igima na Kijiji cha Mpofu, Kijiji cha Ngajengwa (kwa Mtwanga), Kata ya Mchombe na Kijiji cha Igia, Kata ya Mofu na Kijiji cha Ikwambi, Kata ya Mbingu, Kata ya Utengule na Kijiji cha Ipugasa, Kata ya Kamwene na Kata ya Uchindile, Kata ya Msagati Kijiji cha Taweta na Kijiji cha Tanga, Kata ya Kalengakelu na Merela, Kata ya Mlimba - Sokoni na Kata ya Idete – Barabara ya Itikinyu?

Supplementary Question 2

MHE. ZACHARIA P. ISSAAY: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana kwa kunipa nafasi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tatizo la makorongo na mahitaji ya madaraja katika majibo ya vijijini imekuwa kubwa sana na kwa kuwa maeneo haya yanatatiza na kuzuia huduma za jamii nyakati za masika, katika Jimbo la Mbulu Mji kuna Daraja la Gunyoda linalounganisha Halmashauri ya Mbulu Mjini na Halmashauri ya Mbulu Vijijini; mahitaji ya ujenzi wa daraja lile ni zaidi shilingi milioni 600 na kwakuwa fedha tunazopata kutoka TARURA kwenye jimbo la Mbulu Mji ni shilingi milioni 600 na hazitaweza kusaidia ujenzi wa daraja hilo pamoja na maeneo mengine nchini. Je, Serikali haioni sasa ni wakati mwafaka mpango mkakati kwa kuainisha baadhi ya maeneo hayo ili tuweze kutatua tatizo hili linalokwaza jamii katika kupata huduma?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, kama ambavyo Mheshimiwa Mbunge amesema katika swali lake kuna maeneo ambayo yanauhitaji maalum na kiasi cha fedha ambacho kinatakiwa kitumike kingi na yeye mwenyewe katika swali lake anasema kiasi ambacho TARURA Wilayani kwake wanapangiwa kiasi kidogo, ni vizuri tuendelee kushirikiana tuone maeneo hayo ili tuwe na mpango mahususi katika kuhakikisha sehemu ambazo inahitajika fedha nyingi ili kuwe na andiko maalumu kwa ajili ya kutatua maeneo yenye matatizo makubwa kama hayo.

Name

Dr. Pudenciana Wilfred Kikwembe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Kavuu

Primary Question

MHE. SUSAN L. KIWANGA Aliuliza:- Jimbo la Mlimba lina mito mingi mikubwa inayotenganisha kata pamoja na vijiji. Je, ni lini TARURA itajenga madaraja ya kudumu katika Kata ya Mbingu na Kijiji cha Chiwachiwa, Kata ya Igima na Kijiji cha Mpofu, Kijiji cha Ngajengwa (kwa Mtwanga), Kata ya Mchombe na Kijiji cha Igia, Kata ya Mofu na Kijiji cha Ikwambi, Kata ya Mbingu, Kata ya Utengule na Kijiji cha Ipugasa, Kata ya Kamwene na Kata ya Uchindile, Kata ya Msagati Kijiji cha Taweta na Kijiji cha Tanga, Kata ya Kalengakelu na Merela, Kata ya Mlimba - Sokoni na Kata ya Idete – Barabara ya Itikinyu?

Supplementary Question 3

MHE. DKT. PUDENCIANA W. KIKWEMBE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kunipatia nafasi na mimi niulize swali la nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa matatizo yaliyopo Jimbo la Mlimba yanafanana na matatizo yaliyoko katika Jimbo la Kavuu na kwa kuwa nilikwisha omba maombi maalumu kwa ajili ya matengenezo ya daraja linalounganisha Kata ya Chamalemu D na Mwamwamapuli. Je, Serikali sasa ina mpango gani wa kupeleka pesa kwa ajili ya kutengeneza daraja hilo hili wananchi wa maeneo hayo waweze kupata huduma za afya katika Kata ya Kibaoni badala ya kuzunguka Kata ya Mbede?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, ni azma ya Serikali kuhakikisha kwamba tunaondolea adha wananchi ili wasilazimike kuzunguka umbali mrefu wakati ingewezekana kujenga daraja ili wananchi wasitembee umbali mrefu. Naomba nimhaikikishie Mheshimiwa Mbunge ni vizuri baada ya Bunge hili, baada ya kipindi hiki tuwasiliane na coordinator wa Mkoa tujue uwalisia na uhitaji kwa ajili ya daraja hilo ambalo linaweza likajenga ili wananchi wasilazimike kutembea umbali mrefu wakiwa wanafuata huduma ya afya ambayo na yeye mwenyewe anaridhika jinsi ambavyo huduma hii inatolewa kwa karibu, lakini adha imekuwa ni hilo daraja.